Wizara ya mambo ya nje ya India imesema katika taarifa kuhusu ziara ya kansela Friedrich Merz kwamba yeye na mwenyeji wake Narendra Modi watazingatia maendeleo yaliyopatikana katika nyanja mbalimbali za ushirikiano wa kimkakati wa India na Ujerumani, ambao ulikamilisha miaka 25 mwaka jana.

Merz na Modi watajadili kuimarisha ushirikiano katika sekta mbalimbali ikiwemo biashara, uwekezaji, teknolojia, elimu na ulinzi.

Kansela Merz pia anatarajiwa kutembelea Gandhi Ashram, ambayo hapo awali yalikuwa makazi ya Mahatma Gandhi na kitovu kikuu cha mapambano ya India ya uhuru kutoka kwa utawala wa kikoloni wa Uingereza.

Siku ya Jumanne, Merz atatembelea Bengaluru, kitovu cha tasnia ya teknolojia ya hali ya juu ya India.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *