Kwa mujibu wa vyanzo vilivyo karibu na mchakato huo, mazungumzo kati ya Manchester United na Carrick yamepiga hatua kubwa na viongozi wa klabu hiyo wana imani kuwa uteuzi huo utakamilika kabla ya wachezaji kurejea mazoezini siku ya Jumatano.
Ingawa uamuzi wa mwisho bado haujatangazwa rasmi, taarifa zinasema kuwa Carrick, mwenye umri wa miaka 44, yuko mbele ya wagombea wengine na ndiye anayependekezwa zaidi kuchukua nafasi hiyo kwa muda.
Uongozi wa United unataka kuleta utulivu wa haraka ndani ya kikosi baada ya kipindi kigumu chini ya Ruben Amorim, na Carrick anaonekana kuwa chaguo linaloaminika kutokana na historia yake na klabu.
Hii sio mara ya kwanza kwa Carrick kushika usukani wa kikosi cha kwanza.
Historia ya Carrick kama kocha wa muda
Carrick aliwahi kuwa kocha wa muda wa United na alisimamia michezo mitatu tu baada ya kufutwa kazi kwa Ole Gunnar Solskjaer mnamo mwaka 2021. Alishinda mechi mbili na kutoka sare moja kati ya mechi hizo, lakini aliondoka Old Trafford baada ya kuwasili kwa Ralf Rangnick kama kocha wa muda.
Uongozi wa United unaona rekodi hiyo kama ishara ya uwezo wake wa kuongoza timu katika kipindi cha mpito.
Mnamo Januari 5, Manchester United ilimfuta kazi Ruben Amorim baada ya miezi 14 kazini iliyojaa misukosuko. Darren Fletcher, kiungo wa zamani wa United na timu ya taifa ya Scotland, alipewa jukumu la muda la kusimamia kikosi cha kwanza baada ya kuondoka kwa Amorim.
Mashetani hao wekundu walipoteza mchezo wa raundi ya tatu ya Kombe la FA Cup dhidi ya Brighton siku ya Jumapili, katika kile kinachoonekana kuwa mchezo wa pili na wa mwisho kwa Fletcher akiwa kocha wa muda. Aliongoza timu kupata sare dhidi ya Burnley katika mechi ya Ligi Kuu ya Premia Jumatano iliyopita.
Carrick, kiungo wa zamani wa England, alicheza mechi 464 katika mashindano yote akiwa na nyuzi ya United kati ya mwaka 2006 na 2018, baada ya kusajiliwa kutoka Tottenham na Sir Alex Ferguson.
Carrick hajakuwa na kazi tangu Juni alipofutwa na Middlesbrough baada ya miaka miwili na nusu madarakani. Akiwa huko, aliwahi kuiongoza timu hiyo hadi hatua ya mchujo wa kupanda daraja, lakini matokeo yasiyoridhisha msimu uliofuata yakasababisha kuondoka kwake.
Kiungo huyo wa zamani wa England hajakuwa na kazi tangu Juni alipofutwa na Middlesbrough baada ya miaka miwili na nusu madarakani. Akiwa huko, aliwahi kuiongoza timu hiyo hadi hatua ya mchujo wa kupanda daraja, lakini matokeo yasiyoridhisha msimu uliofuata yakasababisha kuondoka kwake.