
Rais wa Marekani Donald Trump amewataka waandamanaji wa Iran kuendelea “kuandamana na kuchukua udhibiti wa taasisi,” akisema kuwa “msaada unakuja,” huku akiwaonya maafisa wa Iran kwamba watalipa gharama kubwa.
“Wazalendo wa Iran, endeleeni kuandamana, chukueni udhibiti wa taasisi zenu!!! Muhifadhi majina ya wauaji na wanyanyasaji. Watalipa gharama kubwa,” Trump aliandika kwenye mtandao wa Truth Social siku ya Jumanne.
Aliongeza kuwa amesitisha mikutano yake yote na wanadiplomasia wa Iran.
“Nimesitisha mikutano yote na maafisa wa Iran hadi mauaji ya kipuuzi ya waandamanaji yakome. Msaada unajuka. MIGA!!! (Ifanye Iran iwe kubwa tena)”
Trump alitumia kauli mbiu yake maarufu ya ‘Make America Great Again’, lakini mara hii ametumia neno Iran badala ya Marekani.
Siku ya Jumatatu, Ikulu ya White House ilisema rais wa Marekani “ana nia” ya kutafuta uwezekano wa kufanya mazungumzo ya diplomasia na Iran.
