Polisi wa Ethiopia wanadai kukamata maelfu ya risasi zilizotumwa na Eritrea kwa waasi katika eneo la Amhara nchini Ethiopia. Eritrea imekusha madai haya, ikiyaita uongo unaolenga kuhalalisha uingiliaji kati wa kijeshi.

Imechapishwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Mashtaka haya ya polisi wa shirikisho la Ethiopia yanazidisha mzozo kati ya Ethiopia na Eritrea, mahasimu wawili wa muda mrefu waliosaini makubaliano ya amani mwaka wa 2018, ambayo tangu wakati huo yamefufua vitisho na uhasama.

Siku ya Jumatano jioni polisi walitangaza katika taarifa kwamba walikamata risasi 56,000 na kuwakamata washukiwa wawili wiki hii katika eneo la Amhara, ambapo waasi wa Fano wamekuwa wakiendesha uasi tangu mwaka 2023.

“Uchunguzi wa awali kuhusu washukiwa wawili waliokamatwa ulithibitisha kwamba risasi hizo zilitumwa na serikali ya Shabiya,” taarifa hiyo ilisema, ikitumia neno la chama tawala nchini Eritrea.

Waziri wa Habari wa Eritrea Yemane Gebremeskel ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba Chama cha Prosperity (PP) cha Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed kilikuwa kinatafuta kisingizio cha kushambulia.

“Utawala wa PP unatumia visingizio vya uongo kuhalalisha vita ambavyo vimekuwa vikitamani kuanza kwa miaka miwili iliyopita,” amesema.

Katika mahojiano na vyombo vya habari vya serikali mapema wiki hii, Rais wa Eritrea Isaias Afwerki alisema kwamba Chama cha Prosperity kilitangaza vita dhidi ya nchi yake. Alisema Eritrea haitaki vita, lakini akaongeza, “Tunajua jinsi ya kutetea taifa letu.”

Nchi hizo mbili zilipigana vita vya mpakani vya miaka mitatu vilivyoanza mwaka wa 1998, miaka mitano baada ya Eritrea kupata uhuru kutoka Ethiopia.

Walitia saini makubaliano muhimu ya kufufua uhusiano mwaka wa 2018, ambayo yalimpatia Rais wa Ethiopia Abiy Ahmed Tuzo ya Amani ya Nobel mwaka uliofuata. Wanajeshi wa Eritrea baadaye walipigana pamoja na jeshi la Ethiopia wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe vya mwaka 2020-2022 katika eneo la kaskazini mwa jimbo la Tigray, kaskazini mwa Ethiopia.

Lakini uhusiano ulizorota baada ya Asmara kutengwa na makubaliano ya amani yaliyomaliza mzozo huo. Tangu wakati huo, Eritrea imekuwa ikikasirishwa na matamshi ya mara kwa mara ya Abiy Ahmed kwamba Ethiopia isiyo na bandari ina haki ya kufikia bahari—taarifa ambazo wengi nchini Eritrea, taifa linalopakana na Bahari Nyekundu, wanaona kama tishio lisilo wazi la kuingilia kijeshi.

Abiy Ahmed amesema kwamba Ethiopia haitafuti mzozo na Eritrea na inataka kushughulikia suala la kufikia bahari kupitia mazungumzo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *