Kenya imesaini makubaliano ya awali ya biashara na China ambayo yangeipa 98% ya mauzo yake ya nje ufikiaji usiotozwa ushuru katika soko kubwa la China, serikali ya Nairobi ilisema Alhamisi, huku makubaliano kamili na ya mwisho yakiendelea.

Imechapishwa:

Dakika 3 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Nchi hii ya Afrika Mashariki imeimarisha uhusiano wake na China, huku Rais William Ruto akifanya ziara ya kiserikali Beijing mwaka jana, ambapo mikataba kadhaa ya ufadhili na ushirikiano ilisainiwa.

“Tumeanzisha mazungumzo na China ili kujadili makubaliano ya biashara ya pande mbili,” wizara ya biashara ya Kenya imesema katika taarifa, ikifichua mazungumzo hayo kwa mara ya kwanza. “Mazungumzo haya yamesababisha makubaliano ya awali.”

Serikali ya China haikujibu mara moja ombi la kutoa maoni.

Makubaliano haya yanatokana na uamuzi wa Beijing wa kuondoa ushuru wote unaotumika kwa mataifa 53 ya Afrika ambayo inadumisha uhusiano wa kidiplomasia nayo, wachambuzi wamesema. Uamuzi huu ulitangazwa mwezi Juni mwaka uliyopita, kufuatia kampeni ya ushuru wa kimataifa iliyozinduliwa na Rais wa Marekani Donald Trump.

“Ili tangazo hili lizingatie sheria za WTO, nchi zenye kipato cha kati kama Kenya lazima zihitimishe mikataba ya biashara ya pande mbili na China,” amesema Hannah Ryder, mwanzilishi wa Development Reimagined, kampuni ya ushauri iliyobobea barani kuhusu Afrika.

Mikataba ya pande mbili hatimaye itakuwa ya pande zote mbili, amesema, lakini nchi za Afrika zitakuwa na muda wa kukuza uchumi wao ili kushindana na viwanda vikubwa ya China.

Kenya, nchi yenye uchumi mkubwa zaidi katika kanda ya Afrika Mashariki, ilikuwa na nakisi ya biashara ya shilingi bilioni 549.82 (dola bilioni 4.27) na Beijing mwaka wa 2024, ikiwa imesafirisha bidhaa zenye thamani ya shilingi bilioni 26.32 pekee kwenda China na kuingiza thamani ya shilingi bilioni 576.14.

Makubaliano ya awali, yaliyofikiwa mwezi uliopita kufuatia mazungumzo ambayo yalikuwa yamebaki kuwa ya siri hadi wakati huo, yanaitwa rasmi “Mkataba wa Mavuno ya Mapema,” kuruhusu bidhaa za Kenya kufikia soko la China huku zikisubiri kukamilika kwa makubaliano ya mwisho.

“Kuanzishwa kwa ufikiaji usiotozwa ushuru kutafungua uwezo mkubwa wa kiuchumi kwa wauzaji nje wa Kenya,” wizara imesema, ikiongeza kuwa makampuni yataweza kusafirisha bidhaa zaidi za kilimo, bila kutaja ni bidhaa zipi.

Majaribio ya awali ya kurekebisha usawa wa kibiashara kati ya nchi hizo mbili, ikiwa ni pamoja na kuruhusu mauzo ya parachichi mbichi za Kenya kwenda China mwaka wa 2022, yameshindwa kupunguza pengo hilo.

Kuchanganya ushirikiano na China na Marekani

Kenya pia ni mshirika wa karibu wa Washington na inajadili makubaliano tofauti ya biashara ya pande mbili na utawala wa Trump, ambayo yamechochea ripoti za hivi karibuni katika vyombo vya habari vya ndani zikipendekeza kwamba uhusiano wa karibu na China unaweza kuikasirisha Marekani.

Maafisa wamekanusha ripoti hizi.

“Hatuoni mvutano wowote kati ya kuhitimisha makubaliano ya upatikanaji wa soko na China, kwa upande mmoja, na juhudi zetu zinazoendelea za kusasisha AGOA na kufuata makubaliano tofauti ya biashara ya pande mbili na Marekani, kwa upande mwingine,” alisema Korir Sing’oei, Katibu Mkuu katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Kenya, kwenye mtandao wa kijamii wa X wiki hii.

Ruto alitetea kuanzishwa kwa uhusiao na China dhidi ya ukosoaji kutoka kwa baadhi ya maafisa wa Marekani, akisema kwamba Kenya ilihitaji kuuza bidhaa zaidi kwa nchi yenye uchumi mkubwa zaidi barani Asia ili kupunguza nakisi ya biashara.

Uhusiano wa kiuchumi kati ya China na Kenya unaenea zaidi ya biashara ya kawaida. China ndiyo mkopeshaji mkubwa zaidi wa pande mbili wa Nairobi, na pande hizo mbili zimekubaliana kubadilisha sarafu ya msingi ya baadhi ya mikopo kutoka dola za Marekani hadi Yuan ya China ili kupunguza gharama za riba.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *