Maadhimisho ya wiki ya huduma za fedha kitaifa yanatarajiwa kufanyika jijini Tanga Januari 19 hadi 26, 2026.
Kwa mujibu wa Wizara ya Fedha, kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni ” Elimu ya Fedha, Msingi wa maendeleo ya Kijamii na Kiuchumi.”
Mgeni rasmi wa maadhimisho hayo yatakayofanyika viwanja vya Usagara anatarajiwa kuwa Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar.
