‎Rais wa Shirikisho la Soka Afrika(CAF), Dkt Patrice Motsepe amefuta mashindano yanayohusu wachezaji wanaocheza Ligi za ndani (CHAN), akidai yanagharimu kiasi kikubwa cha fedha.

‎Motsepe ametoa kauli hiyo kupitia mkutano wake na waandishi wa habari jijini Rabat, Morocco.

‎”Kazi yetu ni kufanya maamuzi yenye maslahi kwa soka la Afrika. CHAN ni mashindano ambayo yanatufanya tupoteze fedha,” amesema.

Motsepe ameongeza kuwa CAF ilihitaji kufikiria upya vipaumbele vyake.

‎Ikumbukwe hilo linakuja baada ya mabadiliko ya michuano ya AFCON kutoka kuchezwa kila baada ya miaka miwili na sasa ikiwa ni kila baada ya. miaka minne.

‎Mashindano ya CHAN mara ya mwisho yalifanyika Afrika Mashariki chini ya nchi tatu, Kenya, Tanzania na Uganda, huku ubingwa ukichukuliwa na Morocco.

#StarTvUpdate

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *