Yanga imeendeleza wimbi la ushindi Ligi Kuu NBC Tanzania Bara wakati huu kichapo kikienda kwa wajeda,Mashujaa FC.
Sio tu Yanga imeshinda na kuondoka na alama tatu bali imetoa na burudani ya mpira, matokeo makubwa.
Kivutio zaidi kwa Wananchi ni straika wao mpya, Maria Depu kutoka Ligi Kuu Poland kufanikiwa kufunga mechi yake ya kwnza, lakini pia akitoa assist.
Kiufundi Yanga pamoja na ushindi mkubwa ambao wameuvuna bado wamecheza mpira wa kitabuni bila kupoteza nishati kubwa sana.
Imecheza objective football. Haijataka kukimbazana sana uwanjani wala kugongana sana, wala kuwa na matamanio kumiliki mali nga nga nga, walistiki kwenye vitu muhimu.
Kwa upande wa Mashujaa ilikuwa na makosa mengi ya kiulinzi hasa kukaba kwa macho, huku ikipoteza mipira mara kadhaa kirahisi wakati wa maandalizi ya shambulizi kutokea katikati ya Uwanja.
Full Time
Yanga 6-0 Mashujaa