
Ni karibu mwaka mmoja tangu Donald Trump arudi Ikulu ya White House. Akikaribia umri wa miaka 80, Rais wa 47 wa Marekani anaonekana kuwa na nguvu zaidi kuliko hapo awali. Na kwa sababu nzuri: nyuma ya uzalendo wake usiozuiliwa kuna motisha za kibinafsi za kutumia nguvu ili kujitajirisha, kupitia mamlaka aliyonayo.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Dakika 4 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Ni nini kinachomsukuma Donald Trump? Upendo wa nchi yake, uhifadhi wa utamaduni wa Marekani, au “hatima iliyo wazi” yote ni majibu ambayo Rais wa 47 wa Marekani huficha matamanio yake binafsi. Mwaka wa mmoja baada ya kurudi kwake madarakani unakaribia kuisha, inakuwa wazi kila siku kwamba utumiaji wa madaraka wa bilionea huyo unaendeshwa na mawazo ya biashara yake, kwa mvuto wa faida, na nia ya wazi ya kuacha alama ya kudumu katika historia.
Tangu mwezi Januari 2025, amepata mikataba mingi yenye faida kwa mashirika makubwa ya Marekani, ambayo mara nyingi hupatikana kupitia majadiliano magumu. Wakati huo huo, utajiri mkubwa wa familia ya Trump umeongezeka tu. Tangu arudi White House, Donald Trump pia amefanya miradi mikubwa ya usanifu na ukumbusho akijitukuza, hata kufikia hatua ya kuandika upya historia kwa niaba yake.
“Tajiri zaidi kuliko hapo awali”
Haikuchukua muda mrefu kwa mfanyabiashara-rais wa Marekani kurejesha sera yake ya kimataifa, iliyokolezwa na “art of the deal”. Baada ya kutawazwa kama rais, alianzisha vita vya kibiashara na washirika wake wakuu wa kibiashara – ambao wengi wao hatimaye walikubali madai yake. Lakini nia ya Donald Trump ya mikataba yenye faida imekuwa isiyotosheka zaidi.
Njia zake za sera za kimataifa mara nyingi huchukua sura ya mvutano, ambapo haogopi kupotosha mkono wa mshirika wake. Lengo mara nyingi huwa sawa: kuipatia Marekani malighafi. Kwa hivyo, mnamo mwezi Aprili 2025, aliweka msingi wa usaidizi wa Marekani kwa Ukraine kwenye mikataba ya madini.
Hali kama hiyo ipo katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambapo Donald Trump aliahidi kuunga mkono vikosi vya Kinshasa dhidi ya makundi yenye silaha badala ya kuundwa kwa “hifadhi ya madini ya kimkakati” kwa matumizi ya Wamarekani waliko nchini humo. Na wakati hakuna makubaliano yanayofikiwa, mfanyabiashara huyo aliye katika Ofisi ya Oval hajishughulishi na diplomasia.
Vita vya ushuru vilivyoanzishwa mwezi Januari 2025 dhidi ya washindani wa biashara, lakini pia dhidi ya washirika, ni mfano wa kushangaza. “Sasa kimsingi kuna upungufu wa uaminifu, kwa sababu ushuru mwingi umetozwa kwa marafiki na washirika wetu wa karibu, haswa nchi zenye madini na metali muhimu ambazo Marekani inahitaji,” mchumi Heidi Crebo-Rediker aliliambia Baraza la Mahusiano ya Kigeni mnamo mwezi Julai. Donald Trump bado hajavunjika moyo.
Kwa hivyo, vitisho vyake vya mara kwa mara dhidi ya Greenland—karatasi ya barafu ya kimkakati ya kudhibiti njia za meli za Aktiki [karatasi ya barafu ni eneo kubwa sana la barafu linalofunika bara na linaweza kufikia unene wa mita elfu kadhaa]—na pia dhidi ya hifadhi zake adimu za ardhi, vimechukua mwelekeo mpya kabisa baada ya kufanya mashambulizi nchini Venezuela na kukamatwa kwa rais wake, Nicolás Maduro. Nyuma ya ahadi ya kumfikisha “mgaidi wa dawa za kulevya” mbele ya sheria kuna akiba kubwa ya mafuta ya nchi hiyo ya Amerika Kusini, inayotamaniwa na Donald Trump. Tangu wakati huo amejivunia makubaliano na viongozi wa mpito wa Venezuela kwa kuipa Marekani mapipa milioni 50.
ExxonMobil, kampuni kubwa ya mafuta ya Marekani, kwa sasa inasita kuwekeza katika nchi hiyo inayokabiliwa usalama mdogo. Lakini Donald Trump, kama kawaida, anajaribu kuwahakikishia wawekezaji wakubwa. Mnamo mwezi Aprili 2025, aliwahakikishia kwenye mtandao wake wa Truth Social kwamba “sera zake hazitabadilika kamwe,” kabla ya kuongeza kwa shauku mpya: “Sasa ni wakati mwafaka wa kutajirika, kutajirika zaidi ya hapo awali!!!”
Na rais Donald Trump anajua vyema hili. Mikataba ya biashara kwa nchi anayoiongoza ni jambo moja. Bahati yake binafsi ni jambo lingine. Katika kipindi cha chini ya mwaka mmoja, imekua kutoka dola bilioni 4.3 hadi zaidi ya dola bilioni 7, kulingana na jarida la Forbes. Ongezeko la starehe la karibu dola bilioni 3. “Hakuna rais katika historia ya Marekani ambaye ametumia nafasi yake ya madaraka kujitajirisha kama [Donald] Trump,” chombo cha habari cha Marekani kinasema.
Fedha za kidijitali, zawadi, na mikataba mikubwa
Ni wapumbavu pekee ambao hawabadilishi mawazo yao. Ukosoaji mkali wa sarafu za kidijitali wakati wa muhula wake wa kwanza, Donald Trump amebadilisha msimamo wake tangu wakati huo. Mnamo 2024, wakati akifanya kampeni ya kurejea Ikulu ya White House, bilionea huyo alianzisha Shirika la Fedha Duniani “World Liberty Financial” (WLF) pamoja na rafiki yake wa karibu Steve Witkoff – ambaye tangu wakati huo amekuwa Mjumbe Maalum wa Marekani Mashariki ya Kati na afisa mkuu wa mawasiliano na Moscow. Watoto watatu wa kiume wa Trump pia wameorodheshwa miongoni mwa wanachama waanzilishi wa kampuni hiyo.
WLF inatoa bidhaa mbili pekee: sarafu mbili za kidijitali, $WLFI na USD1. Hapo awali walisita kuanzisha kampuni hiyo, uwekezaji kutoka kwa majina kadhaa makubwa katika sekta hiyo – ulioanzishwa na Justin Sun – uliongezeka baada ya uchaguzi wa Donald Trump, kwani alikuwa akiunga mkono sana maendeleo ya sarafu za kidijitali wakati wa kampeni yake. Aina hii ya mradi ingemruhusu, kwa nadharia, “kupata fedha bila kushtakiwa kwa ufisadi” badala ya neema za kisiasa, anasema Nathalie Janson, profesa msaidizi wa uchumi katika Chuo Kikuu cha NEOMA Business School.