Rais wa Marekani Donald Trump leo anatarajiwa kutoa hotuba kwa viongozi wa dunia huko Davos, Uswisi, baada ya kusisitiza tena vitisho vyake vya kuchukua udhibiti wa Greenland.

Anatarajiwa kuzungumza katika Jukwaa la Uchumi Duniani, ambapo jana Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alionya kuhusu “mabadiliko kuelekea dunia isiyo na sheria”. Trump amesema kuna “mikutano mingi iliyopangwa kuhusu Greenland”.

Haya yanajiri baada ya kuulizwa katika mkutano na waandishi wa habari Jumanne ni kwa kiwango gani yuko tayari kwenda ili kuipata Greenland, naye akajibu: “Mtajua.”

Kuwasili kwake Davos kunatarajiwa kuchelewa kutokana na “hitilafu ndogo ya umeme” kwenye ndege ya Air Force One.

Wakati huo huo, Waziri wa Viwanda na Rasilimali Asilia wa Greenland, Naaja Nathanielsen, aliiambia BBC: “Hatutaki kuwa Wamarekani, na tumekuwa wazi kabisa kuhusu hilo.”

(Feed generated with FetchRSS)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *