Orodha mpya ya vilabu tajiri zaidi duniani imetangazwa, na Manchester United haipo tena kileleni!
Manchester United iliyoshikilia nafasi ya pili mwaka jana kwa utajiri, na kushikilia nafasi mbili za kwanza kwa zaidi ya miaka 15, mwaka huu imeshuka hadi nafasi ya 8.
Licha ya kuongeza kipato cha jumla kwa asilimia 40, uongozi wa Sir Jim Ratcliff na kampuni ya Ineos umeshuhudia timu hiyo kuporomoka kwa kiwango cha chini zaidi katika historia ya mapato .Hili halijawahi kutokea .
Ijapokuwa mapato ya Manchester United yaliongezeka hadi pauni milioni 692, timu hiyo iliyomaliza nafasi ya 15 msimu uliopita wa ligi kuu ya Uingereza pamoja na kushuka kwa asilimia 45 ya mapato ya matangazo ya mechi zao ndio vyanzo vikuu vya kudidimia kwao.
#StarTvUpdate

(Feed generated with FetchRSS)