
Wito mpya wa umoja miongoni mwa wapinzani wa Kongo umezinduliwa Jumatano, Januari 21, na mbunge wa zamani huko Kinshasa. Ados Ndombasi, mbunge wa zamani aliyechaguliwa katika mkoa wa Kinshasa ambaye alianzisha vuguvugu lake “Mbadala 2028” mnamo mwaka 2024, aliwahutubia wanachama wote wa upinzani moja kwa moja katika ujumbe wa video uliorushwa kwenye mitandao ya kijamii.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Na mwandishi wetu huko Kinshasa, Paulina Zidi
Katika video hiyo, alilaani matumizi mabaya ya madaraka kwa uatawala wa Félix Tshisekedi na kupendekeza kufanyika mkutano mkuu mjini Kinshasa.
“Methali ya Kiafrika inasema: peke yako unaenda haraka, pamoja tunaenda mbali zaidi.” Ados Ndombasi, akiwa amevalia ovaroli zake za kawaida za rangi ya chungwa, aliwahutubia moja kwa moja wapinzani wote wa Kongo. Katika tamko lake, mbunge huyo wa zamani anatoa tathmini ya utawala wa rais wa sasa Félix Tshisekedi na kutaka upinzani kujiunga naye.
“Upinzani si mali ya viongozi wachache, wala si usemi wa kazi za mtu binafsi. Unapaswa kuwa nguvu ya pamoja, muungano wa kiraia na kisiasa unaolenga kuishinikiza serikali kuwajibika. Wapendwa viongozi na wanachama wa upinzani, hebu tuandae mara moja mkutano wa upinzani wa Kongo huko Kinshasa ili kufafanua mkakati wa pamoja, maono ya pamoja, na mifumo ya kuchukua hatua,” Ados Ndombasi anasema.
Upinzani wa Kongo kwa sasa umegawanyika kati ya viongozi waliobaki nchini, kama vile Ados Ndombasi, Martin Fayulu, Delly Sessanga, na Jean-Marc Kabund, na wale ambao walikimbilia uhamishoni: Moïse Katumbi, Joseph Kabila, Augustin Matata Ponyo, Franck Diongo, Claudel Lubaya, na Seth Kikuni.
Wito huu mpya si jaribio la kwanza la kuunganisha upinzani na kuwasilisha upande wa pamoja dhidi ya muungano wa rais, lakini hadi sasa hawajafanikiwa.