Takwimu hii, iliyotolewa na wenzetu kutoka Jarida la Time, inaonyesha hisia ya vurugu za ukandamizaji nchini Iran. Idadi hiyo ya vifo inahuu siku za Januari 8 na 9 pekee, wakati vikosi vya usalama vinadaiwa kukandamiza moja ya maandamano makubwa. Kwa upande wao, mamlaka zimeripoti rasmi vifo 3,117, ikiwa ni pamoja na zaidi ya 2,400 waliouawa wakati wa “shughuli za kigaidi.” 

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Idadi ya vifo kutokana na machafuko ambayo yameitikisa Iran kwa wiki kadhaa inaweza kuzidi 30,000, kulingana na Jarida la Time.

Hadi watu 30,000 waliripotiwa kuuawa na vikosi vya usalama vya Iran mnamo Januari 8 na 9 pekee, wakati nchi hiyo ilishuhudia baadhi ya maandamano makubwa zaidi, vyombo vya habari vya Marekani viliripoti siku ya Jumapili, vikiwanukuu maafisa wawili wakuu wa afya wa eneo hilo.

Katika siku hizo mbili, idadi ya miili ilizidi uwezo wa serikali wa kuiondoa, maafisa walisema. Mamlaka iliishiwa na mifuko ya kuhifadhi miili, na malori yalitumika badala ya magari ya wagonjwa.

Kulingana na shirika la habari la Marekani la Human Rights Activists in Iran (HRANA), kuna vifo 5,495 vilivyothibitishwa, ikiwa ni pamoja na waandamanaji 5,149. Kwa sasa shirika hilo la habari linajaribu kuthibitisha visa vingine 17,031 vinavyoshukiwa.

Kwa kuongezea, watu 7,403 waliripotiwa kujeruhiwa vibaya katika ukandamizaji mkali wa vikosi vya usalama, huku 40,887 wakikamatwa. Wanaharakati wamesisitiza mara kwa mara kwamba kuthibitisha idadi ya vifo ni mchakato unaochukua muda mrefu, hasa kutokana na kuzimwa kwa mtandao wa itaneti, hatua iliyochukuliwa na mamlaka za Iran wiki tatu zilizopita.

Mamlaka imeripoti rasmi vifo 3,117, ikiwa ni pamoja na zaidi ya 2,400 waliouawa katika “shughuli za kigaidi,” kulingana na balozi wa Iran huko Geneva. Tehran imeishutumu Israel na Marekani kwa kuchochea maandamano hayo, ikizihusisha kwa vifo vingi, bila kutoa ushahidi wowote.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *