Gavana mwingine nchini  Nigeria amejiondoa kutoka upinzani na anatarajiwa kujiunga rasmi na chama cha APC, chama tawala, Jumatatu, Januari 26, 2026, kulingana na msemaji wake. Gavana huyu ni Abba Kabir Yusuf, anayeongoza Jimbo la Kano, jimbo la pili lenye watu wengi zaidi nchini Nigeria. Kujiondoa huku kunabadilisha sana tasira ya kisiasa kabla ya uchaguzi mkuu utakaofanyika mapema mwaka wa 2027 nchini Nigeria.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Akiwa na mwandishi wetu huko Abuja, Liza Fabbian

Siku ya Jumapili, Januari 25, Abba Kabir Yusuf aliondoka rasmi katika chama cha upinzani cha NNPP, akisababisha wajumbe 21 wa Bunge la jimbo la Kano na wakuu wa wilaya 44 kujiunga na chama tawala. Ili kuhalalisha uamuzi wake, gavana wa Kano alitaja “malumbani ya ndani chama chao yanayoendelea” na “migawanyiko mikubwa” ndani ya chama. “Nimefikia hitimisho kwamba kujiuzulu kwangu kutoka NNPP ndio uamuzi bora zaidi wa kufanya kwa maslahi ya watu wa Kano,” amewaandikia viongozi wa chama. Mwanzoni mwa wiki iliyopita, Abba Kabir Yusuf alizungumza na Rais Bola Tinubu, akidokeza kwamba huenda hivi karibuni akajiunga na APC, chama chenye idadi kubwa ya watu.

Bola Tinubu anatumia fursa ya makundi mbalimbali ya wafuasi wa vyama vya upinzani kujitenga na vyama hivyo. Hili ni pigo kubwa kwa Rabiu Kwankwaso, mshauri wake wa kisiasa. Gavana huyu wa zamani wa Kano alishinda kwa kishindo katika eneo hilo wakati wa uchaguzi wa rais wa mwaka 2023 na ndiye aliyemsukuma Abba Kabir Yusuf kwenye ugavana, akiwakilisha NNPP.

Hata hivyo, kuasi kwake ni ushindi mwingine kwa Rais Bola Tinubu, ambaye tayari amefanikiwa kuwarudisha magavana wanne kutoka kusini mashariki mwa Nigeria kwenye chama chake, ingawa awali walichaguliwa chini ya bendera ya PDP, chama kikuu cha upinzani nchini Nigeria.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *