
Rais wa Marekani Donald Trump anakusudia “kulazimisha” sera ya Venezuela, hatua ambayo haimpendezi rais wa mpito Delcy Rodriguez, ambaye hapo awali aliridhika kushirikiana na Washington.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Wakati Delcy Rodriguez akionekana kukubali udhibiti wa Marekani ambao Donald Trump alikuwa akitaka kwa Venezuela tangu kuanguka kwa Nicolas Maduro, mvutano unaongezeka tena kati ya Caracas na Washington. Rais huyo wa mpito ameitaka Ikulu ya White House siku ya Jumapili kujiepusha na siasa za nchi yake.
“Imetosha na maagizo kutoka Washington kwa wanasiasa wa Venezuela. Acha sera ya Venezuela ndio itafutie ufumbuzi tofauti zetu na migogoro ya ndani. Imetosha na mataifa ya kigeni,” kiongozi huyo ametangaza katika ujumbe kwa wafanyakazi wa mafuta katika jimbo la mashariki la Anzoátegui. “Imeigharimu jamhuri hii sana kulazimika kukabiliana na matokeo ya ufashisti na msimamo mkali katika nchi yetu,” amesema kwa mshangao.
Makubaliano ya mafuta yaliyotolewa kwa Marekani
Delcy Rodriguez aliapishwa kama rais wa mpito mnamo Januari 5, baada ya Rais wa Kisoshalisti Nicolas Maduro kukamatwa na Marekani katika operesheni ya kijeshi huko Caracas. Kufuatia hili, Donald Trump alitangaza kwamba Washington ilikusudia “kusimamia” Venezuela katika maamuzi hadi hatua nyingine itakapo chukuliwa tena.
Tangu wakati huo, chini ya shinikizo la Marekani, rais huyo wa mpito amesaini makubaliano ya mafuta na Marekani, akaanzisha mageuzi ya kisheria ikiwa ni pamoja na sheria mpya ya hidrokaboni, akawaachilia wafungwa wa kisiasa, na akatoa wito wa makubaliano na upinzani.
Wiki iliyopita, Ikulu ya White House, bila kuweka tarehe, ilitangaza kwamba ilitaka kumwalika Delcy Rodriguez nchini Marekani, baada ya mazungumzo ya simu kati ya Donald Trump na yeye na kauli kadhaa za rais wa Marekani kwa kujipongeza na kujisifu.