
Katika siku za hivi karibuni, wawakilishi wa kijeshi wa Marekani na Ufaransa (Africom na CPA) wamesafiri hadi Abuja, hasa kukutana na uongozi wa NCTC – Kituo cha Kitaifa cha Kupambana na Ugaidi nchini Nigeria – huku Rais Bola Tinubu akisaini mikataba tisa ya pande mbili nchini Uturuki mapema wiki hii, moja ya mikataba hiyo ikizungumzia masuala ya ulinzi.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Na mwandishi wetu maalum huko Lagos, Liza Fabbian
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan alisema kwamba nchi yake iko “tayari kushiriki uzoefu wake katika mapambano dhidi ya ugaidi” na Nigeria.
“Tumetathmini fursa za ushirikiano, hasa kuhusu mafunzo ya kijeshi na ujasusi,” alisema Erdogan katika mkutano wa pamoja na waandishi wa habari na Bola Tinubu.
Wakati wa ziara yao Ankara, maafisa wa Nigeria pia walikutana na wawakilishi wa makampuni kadhaa ya silaha ya nchini Uturuki. Ziara hii ilifanyika chini ya wiki moja baada ya ujumbe wa ngazi ya juu wa Marekani kuzuru Abuja, na huku Marekani na Nigeria zikielezea nia yao ya kuimarisha ushirikiano wa usalama.
Inaonekana Nigeria inashirikiana kikamilifu na nchi hizi mbili, kwani siku ya Jumanne, mkuu wa Kamandi ya Afrika, Jenerali wa Ufaransa Pascal Ianni, alimtembelea Mkuu wa jeshi la Wanamaji la Nigeria kujadili ushirikiano uliopo katika Ghuba ya Guinea. Pia alikutana na mratibu wa Kituo cha Kitaifa cha Kupambana na Ugaidi (NCTC) huko Abuja kabla ya kutembelea makao makuu ya jeshi la ulinzi la Nigeria.