Kwa upande mwingine, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, siku ya Ijumaa alisisitiza kuwa uratibu wa karibu na mashauriano ya mara kwa mara kati ya Uturuki na Iran ni muhimu katika kukabiliana na changamoto za kikanda.

Akizungumza na televisheni ya taifa ya Iran wakati wa ziara yake rasmi mjini Istanbul, Araghchi alisema safari hiyo, iliyopangwa miezi kadhaa iliyopita, inafuatia ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Hakan Fidan, na inalenga kujadili masuala ya mataifa mawili, kikanda na kimataifa.

“Iran na Uturuki ni majirani wakubwa ambao daima wamekuwa wakifanya mashauriano ya karibu. Tuna uhusiano imara katika nyanja za kisiasa, kiuchumi, kijamii na kitamaduni, na tunashauriana mara kwa mara kuhusu masuala ya kikanda,” alisema Araghchi.

Aliongeza kuwa malengo yaliyowekwa na Marekani na wadau wengine yanafanya iwe muhimu kwa nchi hizo mbili kuratibu misimamo yao, kulingana na yanayojiri katika kanda, na kubadilishana mawazo kuhusu namna ya kukabiliana na changamoto zilizopo.

Araghchi anatarajiwa kukutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Hakan Fidan, pamoja na Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, wakati wa ziara hiyo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *