Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi anasema nchi yake iko tayari kuanza tena mazungumzo kuhusu mpango wake wa nyuklia. Rais wa Marekani Donald Trump amekuwa akiongeza shinikizo kwa Iran kuanzisha tena mazungumzo hayo, na utawala wake umetuma meli za kivita katika eneo hilo.

Araghchi alifanya mkutano na wanahabari mjini Istanbul Januari 30. Alisema mara kwa mara kwamba Iran iko tayari kurudi kwenye meza ya mazungumzo. Araghchi alisema: “Bado hatuna mpango wa kukutana na Wamarekani. Kama nilivyosema, tuko tayari kwa mazungumzo ya haki na usawa.”

Vyombo vya habari vya Marekani viliripoti kwamba maafisa huko Marekani wanadai Iran ikomeshe kabisa urutubishaji wote wa madini ya urani. Araghchi alisema shughuli za nyuklia ni “za amani” na kwamba Iran “haijawahi kufuatilia silaha za nyuklia.”

Akizungumzia mashambulizi ya anga dhidi ya vituo vya nyuklia yaliyofanywa na Marekani mwezi Juni mwaka jana, alisema “hali itabadilika sana” ikiwa shambulio jingine litatokea sasa.

Trump alizungumza na waandishi wa habari huko Washington Januari 30 kuhusu kupelekwa kwa Jeshi la Wanamaji, akielezea kama “silaha kubwa.” Alipoulizwa kama atawapa Wairani tarehe ya mwisho ya kufikia makubaliano, alijibu, “Ni wao tu wanaojua.” Aliongeza, “Naweza kusema hivi: Wanataka kufanya makubaliano.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *