Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed amesema kuwa nchi yake haikupokea “senti” yoyote kutoka nchi yoyote ya nje, ili kufanikisha ujenzi wa bwawa la kufua umeme, maarufu kama Grand Ethiopian Renaissance Dam (GERD), akipinga madai ya Rais wa Marekani, Donald Trump kuwa Marekani iliyofadhili mradi huo.
Akihutubia bunge la nchi hiyo, Abiy alisema kuwa ujenzi wa bwawa hilo, ulitekelezwa na vyanzo vya ndani vya Ethiopia.
Bwawa hilo, ambalo limejengwa kwenye mto Nile karibu na mpaka wa Sudan, ndiyo bwawa kubwa la kufulia umeme kwa sasa barani Afrika.
