
Mpwa wa Hasina, Tulip Siddiq, ambaye ni mbunge nchini Uingereza kifungo cha miaka minne, kwenye kesi mbili za ufisadi unaohusiana na mradi wa ujenzi wa mji karibu na mji mkuu wa nchi hiyo, Dhaka.
Jaji Mohammed Rabiul Alam wa Korti Maalum aliwahukumu pia kifungo cha miaka saba wapwa wengine wawili, Azmina Siddiq na Radwan Mujib Siddiq kwa kuhusika kwao kwenye ufisadi huo.
Taasisi ya kupambana na ufisadi ya Bangladesh ilifunguwa kesi kwenye mahakama hiyo ikimtuhumu Hasina kushirikiana na maafisa wa serikali kujipatia viwanja sita vya nyumba kwa ajili yake na familia yake kwenye Mradi wa Mji Mpya wa Purchaba, licha ya kwamba hawakuwa na haki kisheria.
Hukumu hiyo imetolewa wakati serikali ya mpito inayoongozwa na mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Muhammad Yunus, ikijitayarisha kwa uchaguzi mkuu hapo Februari 12, ambao chama cha Hasina, Awami League, kimezuiwa kushiriki.