Ousmane Dillo amerejea Sudan. Akiwa amejeruhiwa kutoka El-Fasher, Darfur, miezi michache iliyopita, mbabe huyo wa vita na kaka wa kiongozi wa upinzani wa Chad, Yaya Dillo, amevaa sare yake tena na kujiunga tena na mapigano pamoja na jeshi la Sudan. Kwa sasa inaaminika yuko Kordofan, kitovu cha vita vya wenyewe kwa wenyewe vimeitumbukiza nchi hiyo katika mzozo mkubwa kwa karibu miaka mitatu.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Video hiyo imekuwa ikisambaa kwenye programu za kutuma ujumbe kwa siku chache. Inamuonyesha Ousmane Dillo akitabasamu, akiwa amevaa sare ya rangi ya mchanga akiwa bendera ya Sudan mkononi mwake. Anakaribishwa na wapiganaji waliojihami kwa silaha nzito chini ya gari la kijeshi. Vyanzo kadhaa vinatuthibitishia kwamba amerudi Sudan.

Mwanzoni mwa mwezi Novemba, wakati Vikosi vya Msaada wa Haraka vya Jenerali Hemedti (RSF) kuchukua udhibiti wa El-Fasher, Ousmane Dillo, akiwa amejeruhiwa, alirudishwa N’Djamena, Chad. Baada ya kupata matibabu nchini India, kisha, kulingana na washirika wake wa karibu, alifany wiki kadhaa nchini Saudi Arabia na kisha Misri – nchi mbili zinazoshirikiana na jeshi la Sudan – kabla ya kufika Port Sudan na kisha kuelekea kusini. Kulingana na chanzo cha kuaminika, kwa sasa yuko Kordofan, mashariki mwa Babanusa, katika eneo linalozozaniwa.

Ousmane Dillo ni kiongozi maarufu katika jamii ya Zaghawa, ambayo ina mgogoro wa muda mrefu na wanamgambo wa Hemedti, Janjaweed, ambao sasa wanajulikana kama RSF. Uhusiano wake na binamu yake, Rais wa Chad Mahamat Idriss Déby, pia una matatizo. Alikata rufaa kwa Umoja wa Mataifa na kuwasilisha malalamiko nchini Ufaransa kufuatia kifo cha kaka yake, Yaya Dillo, katika shambulio dhidi ya makao makuu ya chama cha PSF huko N’Djamena mnamo Februari 28, 2024.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *