
Marcus Rashford, 28, hataki kurejea Manchester United mkataba wake wa mkopo Barcelona utakapokamilika na mshambuliaji huyo wa Uingereza yuko tayari kupunguziwa mshahara ili kusalia. (Mirror)
Beki wa Ufaransa Dayot Upamecano, 27, anatarajiwa kusaini mkataba mpya katika klabu ya Bayern Munich. (Fabrizio Romano)