Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer na Rais wa Marekani Donald Trump wamekubaliana siku ya Jumanne, Februari 3, “kuendelea kufanya kazi kwa karibu” ili kuhakikisha operesheni endelevu ya kambi ya pamoja ya kijeshi ya Marekani na Uingereza ya Diego Garcia, katikati ya Visiwa vya Chagos. Makubaliano haya yamethibitishwa tena baada ya wiki kadhaa za mvutano wa kidiplomasia.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Viongozi hao wawili walizungumza kwa simu siku ya Jumanne, Februari 3. Kufuatia mazungumzo haya, Downing Street imebainisha kwamba walikubaliana “kuendelea kufanya kazi kwa karibu pamoja” ili kuhakikisha mustakabali wa kambi hii ya kimkakati katika Bahari ya Hindi.

Katika taarifa tofauti, msemaji wa Waziri Mkuu wa Uingereza alibaiisha kwamba “kuhusu Diego Garcia, na makubaliano yaliyofikiwa na Uingereza ya kudumisha udhibiti wa kambi ya kijeshi ya Marekani na Uingereza ili kulinda usalama wa taifa, viongozi hao walitambua umuhimu wake wa kimkakati.”

Mkataba nyeti kisiasa

Mkataba huo, unaokadiriwa kugharimu pauni bilioni 35 (euro bilioni 40) katika karne ijayo, unaeleza kwamba Uingereza itarudisha Visiwa vya Chagos kwa Mauritius lakini itahifadhi mkataba wa miaka 99 wa kukodisha kisiwa kikuu, Diego Garcia, ili kudumisha kambi ya pamoja ya kijeshi ya Marekani na Uingereza katika eneo hili la kimkakati.

Mnamo mwezi Januari, Donald Trump alikosoa uamuzi wa Uingereza wa kuirudishia kwa Mauritius, Visiwa vya Chagos, visiwa katika Bahari ya Hindi ambapo kambi hii ya kimkakati inapatikana. “Kitendo cha Uingereza kurejesha ardhi muhimu sana ni kitendo cha UJINGA MKUBWA, na kinaongeza orodha ndefu sana ya sababu za usalama wa taifa ambapo Greenland lazima ipatikane,” rais wa Marekani alilaani kwenye mtandao wake wa Truth Social.

Keir Starmer kisha alitangaza kwamba mabadiliko haya ya msimamo yalikusudiwa “kumtia shinikizo (yeye) na Uingereza”, wakati ambapo, kama nchi zingine za Ulaya, alionyesha kuunga mkono kwake Greenland dhidi ya nia ya rais wa Marekani ya kunyakua eneo hili la Denmark.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *