Uturuki na Saudi Arabia zimethibitisha tena kuunga mkono mamlaka kamili na uhuru wa mipaka ya Somalia, na kukataa kile walichokiita hatua za kujitenga na mifumo sambamba inayotishia umoja wa taifa hilo la Pembe ya Afrika. Haya yaliangaziwa wakati Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, alipokutana na Mwanamfalme Mohammed bin Salman mjini Riyadh katika ziara yake rasmi ya siku moja.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Uturuki iliyotolewa Jumatano, viongozi hao wawili katika mkutano wao uliofanyika siku ya Jumanne jijini Riyadh walisisitiza “uungaji mkono thabiti” kwa umoja wa nchi ya Somalia na kwa kuimarisha utulivu, maendeleo na ustawi wa wananchi wake.

Pia walilaani hatu ya Israel kuitambua eneo lililojitenga la Somaliland kama taifa huru na vilevile Somaliland kuitambua Israel kama taifa huru, wakisema kuwa hatua hiyo inaendeleza vitendo vya upande mmoja vya kujitenga, inakiuka sheria za kimataifa na inaongeza mvutano wa kikanda.

Mwishoni mwa Disemba mwaka jana, Israel ilitangaza kuwa imeitambua Somaliland kama taifa huru.

Somaliland imekuwa ikijiendesha kama eneo lenye mamlaka ilipotangaza kujitenga na Somalia mwaka 1991. Hata hivyo, haijapata kutambuliwa rasmi kimataifa, huku serikali ya shirikisho ya Somalia ikisisitiza mara kwa mara kuwa eneo hilo ni sehemu isiyotenganishwa ya ardhi yake.

Msaada wa pamoja kwa serikali halali ya Yemen

Kuhusu suala la Yemen, Uturuki na Riyadh zilisisitiza kuunga mkono kwao serikali halali ya nchi hiyo, inayowakilishwa na Baraza la Uongozi wa Rais na serikali ya Yemen. Pia walisisitiza umuhimu wa kulinda mamlaka, umoja na uhuru wa mipaka wa Yemen.

Upande wa Uturuki uliunga mkono nafasi ya Saudi Arabia nchini Yemen pamoja na juhudi zinazoongozwa na mkuu wa Baraza la Uongozi wa Rais katika kutatua mgogoro na kufanikisha maridhiano ya kitaifa, ikiwemo wito wa kuitishwa kwa mkutano jumuishi jijini Riyadh utakaowaleta pamoja makundi yote ya eneo la kusini mwa Yemen.

Kulinda umoja wa Sudan

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *