
Wajumbe kutoka Ukraine, Urusi, na Marekani wamenza tena mazungumzo huko Abu Dhabi kwa duru ya pili ya mazungumzo yenye lengo la kutafuta suluhisho la vita nchini Ukraine. Baada ya duru ya kwanza ambayo haikuzaa matunda mnamo Januari 23 na 24, ni vigumu kufikiria maendeleo makubwa kuelekea amani wakati wa mazungumzo haya.
Imechapishwa:
Dakika 3 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Mazungumzo yanatarajiwa kuwa magumu tena. Volodymyr Zelensky tayari ameonyesha msimamo wake: baada ya mashambulizi makali ya Urusi dhidi ya Ukraine katika siku za hivi karibuni, “inaonekana kwamba Moscow haichukui njia ya kidiplomasia kwa uzito.” Kazi ya ujumbe wa Ukraine huko Abu Dhabi “itaendana na kiwango.”
Itaendana na kiwango, bila shaka, kuwa rahisi kubadilika, hasa kwa kuwa mazungumzo bado yamekwama kwenye suala moja: eneo. Urusi inakataa kurudi nyuma kutokana na madai yake na inasisitiza kuhusu eneo lote la Donbas. Suala ambalo linaonekana kuwa i mstari mwekundu kwa rais wa Ukraine, ambaye anapendekeza kwamba suala la mpaka haliwezi kutatuliwa bila mkutano wa pande mbili na Vladimir Putin.
Kwa upande wake, Rais wa Marekani Donald Trump alirudia kusema Jumanne, Februari 3, kwamba Vladimir Putin anataka kukomesha vita nchini Ukraine, jambo ambalo alisisitiza usiku wa kuamkia mazungumzo na wajumbe wake Steve Witkoff na Jared Kushner.
Wakati huo huo, wanajeshi wa Urusi wanasinga mbele kwenye mstari wa vita. Usiku wa Jumatatu, Februari 2, kuamkia Jumanne, Februari 3, baada ya usitishaji mfupi wa mahambulizi, Moscow ilirusha mamia ya ndege zisizo na rubani na idadi kubwa ya makombora ya balestiki nchini Ukraine, na hivyo kukata mfumo wa upashaji joto kwa miji kadhaa kote nchini. Na kulingana na Taasisi ya Utafiti wa Vita, mnamo mwezi Januari Urusi iliteka maeneo mengi ya Ukraine mara mbili ya mwezi uliopita.
Falme za Kiarabu, mpatanishi mwenye uzoefu katika mazungumzo kati ya Ukraine na Urusi
Falme za Kiarabu tayari zilikuwa ziliandaa raundi ya kwanza ya mazungumzo kati ya Urusi na Ukraine mwishoni mwa mwezi Januari. Na hii si mara ya kwanza nchi hiyo kuwezesha majadiliano kati ya pande hizo mbili. “Baada ya uchokozi wa Urusi dhidi ya Ukraine, Imarati ilipenekeza kwa pande zote mbili ili kuchukua jukumu la upatanishi, na walichagua suala litakaopewa kipaumbele: wafungwa. Ndiyo maana Imarati ilianza upatanishi wake mapema sana ili kuhakikisha kuachiliwa kwa baadhi ya wafungwa wa Urusi walioshikiliwa na wanajeshi wa Ukraine na wanajeshi wa Ukraine walioshikiliwa na Warusi,” anabainisha Hasni Abidi, mkurugenzi wa Dermam, Kituo cha Mafunzo na Utafiti katika ulimwengu wa Kiarabu na Mediterania, huko Geneva.
Upatanishi wa kwanza ulifanyika mnamo Agosti 24, 2025. Lakini tangu wakati huo, kumekuwa na kasi inayoonekana ya upatanishi huu. Leo, tunazungumzia kuhusu patanisho 17 za Imarati ambazo zimetoa matokeo chanya.
Falme za Kiarabu zinaweza kuchukua jukumu hili la upatanishi kwa sababu zimedumisha uhusiano mzuri na Urusi, anabainisha Hasni Abidi. “Kuna ufikiaji huru, tofauti na nchi kadhaa katika eneo hilo, mataifa ya Ulaya ambayo yanaweka vikwazo vikali, hasa dhidi ya raia wa Urusi, mali za Urusi, na biashara na Urusi. Hakuna kitu cha aina hiyo kilichopo katika Falme za Kiarabu, licha ya, bila shaka, mahitaji ya Ulaya na Marekani. Na haswa ili kusawazisha uhusiano huu na Urusi, Imarati mara moja ilitoa msaada wao wa kibinadamu, matibabu, kijamii, na kielimu kwa Ukraine.”
“Saudi Arabia inadumisha uhusiano mzuri na Moscow, lakini ni Imarati ambayo inaonekana kama kimbilio salama, hasa kwa viongozi wa Urusi, lakini pia katika suala la mabadilishano ya kiuchumi kati ya nchi hizo mbili”, ameongeza Hasni Abidi, Mkurugenzi wa Dermam.