Zaidi ya watu milioni 3 wamerejea nyumbani kwa nhcini Sudan Kusini. 

Kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji IOM wengi wa watu wanaorejea nyumbani wamekuwa wakienda moja kwa moja kwenye maeneo yao ya awali au maeneo ya jirani kuanza maisha upya.

media:entermedia_image:99e05d1a-1633-4608-97e8-770bafe48d10

Familia zinarudi kwenye uharibifu, karibu miaka mitatu katika mzozo. Maeneo mengi ya kurudi yana uharibifu mkubwa wa makazi, huduma za msingi, na miundombinu muhimu.

Familia zinarejea kwenye hali uharibifu wa kiwango cha juu baada ya takribani miaka mitatu ya vita

Mazingira yako taabani, nyumba zimebomolewa, huduma za msingi zimesambaratika, na miundombinu muhimu inahitaji ukarabati mkubwa.

media:entermedia_image:3d044e98-688c-4b68-8507-f0ea9bfbac14

Wengi waliorejea walikuwa wakimbizi wa ndani nchini humo hapo awali. Takriban 83% ya waliorejea walitoka ndani ya Sudan, wakati 17% walirejea kutoka nje ya nchi.

Watu wengi wanaorejea walikuwa wakimbizi wa ndani

Asilimia 83 ya watu wanaorejea wametokea ndani ya Sudan, huku asilimia 17 pekee ndio wanaotokea nchi jirani na kurejea makwao. 

media:entermedia_image:e40bb296-3a62-4320-afb5-ccb080761dd5

Maeneo ya kurudi yanahitaji makazi kwa dharura na ujenzi upya.

Jamii zinazowapokea ndizo zinazobeba mzigo mkubwa wa kutoa msaada na huduma

IOM inasema familia zinarejea zikiwa na mizigo kidogo na zingine bila chochote na zikiwa uwezo mdogo sana wa kifedha, jambo linalozidisha hatari ya kupata madhara kutokana na kulemewa kwa miundombinu.

media:entermedia_image:7833a6da-ee26-4c48-bce2-12da7e703d2e

Uhamishaji bado unazidi kuwa mbaya katika maeneo yenye migogoro.

Maeneo wanayofikia yanahitaji kujengwa upya ili kufaa kwa makazi 

Maeneo hayo yanahitaji ujenzi wa dharura wa makazi, mifumo ya maji, shule, na vituo vya afya ambavyo kwa sasa vimezidiwa na wagonjwa. 

media:entermedia_image:053251dd-0079-4fe8-b60e-78ed43e8c1c8

© IOM/Philippa Lowe

Maelfu bado wamenaswa katika miji ya Kordofan, Darfur na El Fasher, ambako vita vinaendelea kupamba moto.

Hali ya watu kufurushwa bado ni mbaya katika maeneo yenye migogoro

Wakati wakirejea nyumbani, ghasia zimezidi kuongezeka huko jimboni Darfur na Kordofan na kusababisha maelfu ya wakimbizi hususan wa ndani kuongezeka. 

media:entermedia_image:edc01a23-1ab7-4ef4-b7b6-68b4a54cda06

IOM inatoa makazi na maji miongoni mwa huduma nyingine muhimu kwa maeneo yanayofikika.

Watoa huduma wa IOM wanaonesha juhudi

Timu za Shirika la Umoja wa mataifa la uhamiaji (IOM) zimekuwa zikitoa hifadhi, maji, na huduma nyingine muhimu katika maeneo yote yanayoweza kufikika kwa usalama.

media:entermedia_image:4bdcc00d-dd0d-492e-9700-7b88fb710349

© IOM/Muse Mohammed

Sudan bado ni janga kubwa zaidi la watu kuhama makazi yao. Hata kwa kurudi, zaidi ya watu milioni tisa wamesalia kuwa wakimbizi wa ndani nchini.

Machafuko nchini Sudan bado ni chanzo kikubwa cha wakimbizi duniani 

Zaidi ya watu milioni 9 wamebaki kuwa wakimbizi wa ndani nchini Sudan licha ya baadhi ya familia kuanza kurejea makwao na mamilioni wengine wamekimbilia nchi jirani.

media:entermedia_image:fe98e06d-5808-4c79-bc95-abf91f958d9e

© IOM/Fedza Lukovac

Sudan bado ni janga kubwa zaidi la watu kuhama makazi yao. Hata kwa kurudi, zaidi ya watu milioni tisa wamesalia kuwa wakimbizi wa ndani nchini.

Msaada unahitajika ili kujenga upya maisha yao

Msaada zaidi unahitajika sasa ili kuwasaidia kujenga upya maisha yao kwani mahitaji yamezidi rasilimali zilizopo nchini humo. 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *