Jamii imehimizwa kuendelea kupinga vikali ukatili wa kijinsia ambao bado umeendelea kusababisha matokeo hasi katika jamii na kutatiza ndoto za wengi kutokana na athari za matukio hayo.
Wito huo umetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la WILDAF Tanzania, Anna Kulaya, wakati wa utoaji wa tuzo kwa vinara 16 waliopinga ukatili wa kijinsia kwa mwaka 2025 zilizofanyika jijini Dar es Salaam, huku baadhi ya washindi wa tuzo hizo wakieleza umuhimu wa kila mtu kuwa mlinzi wa mwenzake kwa kutoa taarifa ya viashiria vyovyote vya ukatili wa kijinsia kwa mamlaka husika ili kusaidia kudhibiti vitendo hivyo.
AzamTVUpdates
Mhariri | John Mbalamwezi