
Kulingana na Ofisi ya Mikakati na Bajeti ya Uturuki (SBB), nchi hiyo imetumia lira trilioni 3.6 za Uturuki (takriban dola bilioni 91.5 za Marekani) katika jitihada za ujengaji upya ndani ya miaka mitatu iliyopita, huku Kahramanmaras na Hatay zikichukuliwa kuwa kitovu cha ujengaji upya.
Makazi yalipatiwa kipaumbele, na nyumba 433,667 na sehemu 21,690 za kazi ziligawanywa kupitia bahati nasibu, huku ujenzi wa makazi ya kudumu ukikamilika.
Mabillioni ya pesa pia imetumika kwenye elimu, afya, miundombinu, nishati, usafirishaji na msaada wa ajira katika mikoa 11.
Ofisi ya SBB imesema kuwa ujengaji upya umekamilika kwa kiwango kikubwa baada ya jitihada za muda mrefu na za kina, na maendeleo makubwa yamefikiwa katika kurejesha huduma za umma, shughuli za kiuchumi, na maisha ya kijamii katika eneo lililoathiriwa na tetemeko la ardhi.