Katika taarifa, msemaji wa Kamati ya Uchunguzi Svetlana Petrenko, amesema Alekseyev alipigwa risasi mara kadhaa na washambuliaji wasiojulikana katika jengo moja la makazi kaskazini magharibi mwa moscow na baadaye kukimbizwa hospitalini.

Hata hivyo Petrenko hakutaja aliyehusika katika shambulizi hilo dhidi ya Alekseyev ambaye amehudumu kama naibu mkuu wa idara ya kijasusi ya Urusi tangu 2011.

Tukio hilo linakuja siku moja tu baada ya wajumbe wa Urusi, Ukraine na Marekani kumaliza mazungumzo ya siku mbili Abu Dhabi yaliyolenga kumaliza mzozo Ukraine ambao umedumu kwa takriban miaka minne.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *