Shirikisho la Soka la Morocco (FRMF) limekanusha vikali taarifa zinazosambaa mitandaoni zikidai kuwa kocha wa timu ya taifa, Walid Regragui, ametoa pendekezo la kujiuzulu kufuatia kipigo cha fainali ya AFCON dhidi ya Senegal.
FRMF imesisitiza kuwa taarifa hizo si za kweli na kwamba Regragui bado yuko kazini na ataendelea kuiongoza timu ya taifa.