
Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amezungumza kwa simu siku ya Jumanne, Februari 10, na mwenzake wa Urusi, Vladimir Putin. Miongoni mwa mada zilizojadiliwa kati ya wakuu hao wawili wa nchi ni hatima ya Waafrika Kusini walioajiriwa katika vikosi vya Urusi na kupelekwa kwenye mtari wa mbele nchini Ukraine. Ingawa nchi kadhaa za Afrika zinaikosoa serikali ya Urusi waziwazi, Afrika Kusini inabaki kuwa mwangalifu zaidi.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Mazungumzo kati ya Cyril Ramaphosa na Vladimir Putin yalilenga hasa maendeleo ya ushirikiano kati ya Urusi na Afrika Kusini katika siku zijazo. Katika taarifa iliyotolewa siku ya Jumanne, Februari 10, rais wa Afrika Kusini alithibitisha tena “uungaji mkono usiyotetereka wa Afrika Kusini kwa juhudi za kidiplomasia na za amani zinazolenga kukomesha mzozo wa Urusi na Ukraine.”
Watu hao wawili walikubaliana kuhusu kurejeshwa nyumbani, haraka iwezekanavyo, kwa raia wa Afrika Kusini walioko Urusi ambao waliandikishwa kushiriki katika juhudi za vita. Kwa upande wake, Kremlin, katika taarifa fupi sana, haikutaja mada hii, ambayo ilijadiliwa wakati wa mazungumzo ya simu.
Waafrika Kusini wanaoishi Urusi “wanalazimishwa” kujiunga na jeshi
Mwezi Novemba mwa uliyopita, Pretoria iliripoti kupokea simu za kuomba msaada kutoka kwa raia wake 17 “waliolazimishwa” kujiunga na jeshi wakati wakisafiri kwenda Urusi kwa kazi. “Timu kutoka nchi zote mbili zitaendelea na majadiliano yao ili kukamilisha mchakato huo,” taarifa hiyo ilioneza.
Afrika Kusini ina tahadhari na nchi ambayo uhusiano wake unatarajiwa kuimarika. Kenya, kwa upande mwingine, ambayo baadhi ya raia wake wameuawa kwenye mstari wa mbele, itatuma waziri wake wa mambo ya nje huko Moscow katika wiki zijazo ili kufafanua hali hiyo.