Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini DRC, MONUSCO, unaendelea na maandalizi yake ya kuanzishwa kwa utaratibu wa ufuatiliaji wa uwezekano wa kusitisha mapigano ambao unaweza kufuata mipango ya hivi karibuni ya kidiplomasia. Kaimu mkuu wa MONUSCO, Vivian van de Perre, alikuwa Goma kwa saa 48 zilizopita kukutana na pande mbalimbali zinazohusika.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Vivan van de Perre aliwasili katika uwanja wa ndege wa Goma kwa helikopta. Hii ilikuwa ishara kubwa, kwani uwanja wa ndege ulikuwa umefungwa kwa zaidi ya mwaka mmoja tangu jiji hilo lilipotekwa na kundi la wasi la AFC/M23. MONUSCO ilisisitiza hili kama hatua muhimu ya uendeshaji, kwani inarejesha udhibiti wa kituo chake katika uwanja huo wa ndege.

Kaimu mkuu wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa alielezea kwamba alikuwepo ili kuendeleza usaidizi wa utaratibu wa ufuatiliaji wa kusitisha mapigano ambao MONUSCO inatakiwa kutoa.

Van de Perre alikutana na pande mbalimbali zinazohusika, ikiwa ni pamoja na viongozi wa AFC/M23. Majadiliano haya yalilenga hasa utekelezaji halisi wa utaratibu huu wa ufuatiliaji, kwa mujibu wa makubaliano yaliyosainiwa na kundi lenye silaha huko Doha, aliwaambia waandishi wa habari.

“Ni muhimu kwamba ahadi zilizotolewa katika makubaliano haya zitafsiriwe haraka katika mipango ya uendeshaji iliyo wazi, inayoaminika, na inayoweza kuthibitishwa,” alisema.

Kaimu mkuu wa MONUSCO pia alitangaza kwamba misheni ya awali ya upelelezi wa angani itatumwa Uvira katika siku zijazo.

“Nimefanya mkutano na mwakilishi wa AFC/M23” ‘ alisema Vivian van de Perre, Kaimu mkuu wa MONUSCO.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *