Mkutano wa 39 wa Umoja wa Afrika sasa umekamilika. Kwa siku mbili, wakuu wa nchi na serikali, wanachama wa Umoja wa Afrika, walijadili migogoro mikubwa inayoathiri bara hilo. Rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye, ambaye alichukua nafasi ya uenyekiti wa kupokezana wa AU katika mkutano huu, na Mwenyekiti wa Tume, Rais wa Djibouti Mahmoud Ali Youssouf, waliwasilisha hitimisho kuu katika mkutano wa mwisho na waandishi wa habari siku ya Jumapili, Februari 15.

Imechapishwa:

Dakika 3 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Umoja wa Afrika hautakuwa na “uvumilivu wowote kwa mapinduzi ya kijeshi kinyume cha katiba,” alitangaza Mwenyekiti wa Tume Mahmoud Ali Youssouf, huku kiongozi wa Guinea Jenerali Mamadi Doumbouya na Rais wa Gabon Jenerali Brice Clotaire Oligui Nguema wakishiriki katika mkutano huo na michakato ya mpito inaendelea Guinea-Bissau na Madagascar, ikifuatiliwa na “wajumbe maalum” wa AU.

Kuhusu nchi za Muungano wa Mataifa ya Sahel (ESA) – Mali, Niger, na Burkina Faso – Umoja wa Afrika unakusudia kudumisha mazungumzo na serikali za kijeshi zilizochukua madaraka, anaripoti mwandishi wetu maalum huko Addis Ababa, David Baché. Kwa Mwenyekiti wa Tume ya AU Mahmoud Ali Youssouf, anasema, “kuongezeka kwa makundi ya kigaidi” katika Sahel kwa kweli ni “tatizo kubwa zaidi.”

Mwenyekiti mpya wa Umoja wa Afrika, Rais wa Burundi, Évariste Ndayishimiye, alikuwa tangu mwezi Julai 2025 “Mjumbe Maalum” wa AU kwa Sahel. Ingawa hajaunganisha tena nchi hizi za ESA katika Umoja wa Afrika, anatumai kuchangia katika mapambano yao dhidi ya makundi ya wanajihadi. “Tunahitaji kujenga mshikamano miongoni mwa nchi za eneo hilo ili kuweka nguvu pamoja kutokomeza makundi haya ya wanajihadi. Hilo ndilo AU inafanya ili kuwasaidia. Viongozi wa mataifa haya pia wanahitaji kufikiwa ili kutafuta kurejea haraka kwa utaratibu wa kikatiba na kuwasaidia kuleta utulivu katika nchi zao. Umoja wa Afrika umedumisha mawasiliano na mataifa ya Sahel ili kufanya kazi pamoja ili kupata suluhu.”

Kwa hivyo, kuundwa kwa “jukwaa la pamoja” la nchi kumi na nane kuhusu masuala ya usalama kumetangazwa kwa “wiki zijazo,” bila maelezo zaidi. Wakuu wa majesh ya ECOWAS, “nguzo” ya Umoja wa Afrika, ambayo mataifa ya ESA yalijiondoa, wamepangwa kukutana Freetown, Sierra Leone, kuanzia Februari 24 hadi 27 ili kubaini ushiriki wao katika kikosi cha  kikanda cha kupambana na ugaidi.

“Kukomesha mapigano” 

Umoja wa Afrika pia unasema “umeazimia kukomesha mapigano ya aina yoyote.” Sio migogoro yote inayoharibu bara hilo iliyotajwa. Hakuna neno lolote kuhusu Sudan, hasa kutoka kwa urais wa mzunguko wa AU au Mwenyekiti wa Tume. Kwa upande wake, mkuu wa Idara ya Masuala ya Siasa, Amani na Usalama ya AU, Adeoye Bankole, alizungumzia suala la vita nchini Sudan, anaripoti mwandishi wetu huko Addis Ababa, Marlène Panara. “Ninarudia: uthabiti ni muhimu sana. Lazima tuhakikishe upatikanaji wa kibinadamu na uratibu wa kimataifa wa mipango.” Pia ni muhimu kuhakikisha kwamba athari katika maeneo ya mipaka haziathiri utulivu wa nchi jirani za Sudan.

Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu imekamilisha uchunguzi wake kuhusu matukio nchini Sudan na kutoa mapendekezo yenye nguvu sana, lakini Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika bado halijazingatia mapendekezo haya au kuyafanyia kazi, ” amesema Laetitia Bader kutoka shirika la kimataifa la haki za bindamu la Human Rights Watch.

Mwanadiplomasia huyo alijibu ukosoaji ulioelekezwa kwa Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika. Ukosoaji huu unaangazia ukosefu wake wa nguvu unaoonekana mbele ya migogoro mingi inayoendelea barani humo: “Changamoto ziko na zinaendelea, nakiri hilo, lakini Baraza halikwepi majukumu yake.” Baraza linafaya kazi, licha ya kasoro ndogo ndogo, na wanachama wake hufanya misheni mbalimbalii katika karibu kila nchi inayokabiliwa na ukosefu wa utulivu, ikiwa ni pamoja na Sudan mnamo mwezi Oktoba 2024.

Alipoulizwa kuhusu vita mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Mwenyekiti mpya wa AU, Evariste Ndayishimiye, alisisitiza umuhimu wa kutekeleza Makubaliano ya Amani ya Washington, na Mwenyekiti wa Tume, Mahmoud Ali Youssouf, alisema kwamba Umoja wa Afrika “umewekwa” “kuongoza” upatanishi, bila kuwaachia washirika wa nje.

“Tunahitaji kikosi cha upatanishi, lakini pia kwa wapiganaji kupitia mchakato wa kuwapokonya silaha na kuwarejesha katika maisha ya kiraia”, amesema Rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *