
Mtoto wa Shah aliyeondolewa madarakani, Reza Pahlavi, ametoa wito tena kwa Donald Trump kwa kuingilia kati kijeshi “haraka” nchini Iran na akarudia pendekezo lake la kuhakikisha “mpito” wa kisiasa nchini Iran, akizungumza kwenye Fox News siku ya Jumapili, Februari 15.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
“Natumai rais anaelewa jinsi uingiliaji kati wa haraka unavyoweza kuokoa maisha na kutusaidia kukomesha utawala huu usiohitajika,” ametangaza Reza Pahlavi, aliye uhamishoni nchini Marekani ambaye amekuwa akiongeza wito wake wa uhamasishaji dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu katika siku za hivi karibuni.
“Mahitaji ya kwanza ya Wairan, ndani na nje ya nchi, ni kuomba msaada,” aliongeza. “Uingiliaji kati huu ni wa kibinadamu, unaokusudiwa kuokoa maisha ambayo vinginevyo yataendelea kupotea.”
Kama “kiongozi wa mpito,” Reza Pahlavi alipendekeza siku ya Jumapili “kuhamasisha na kuunganisha upinzani wa kidemokrasia na usioegemea dini, ujikite kwene utawala wa kikatiba au jamhuri, ili masuala haya yaweze kujadiliwa kwa njia ya kujenga, huku ukiruhusu Wairan wengi kuamua mustakabali wa Iran kupitia mchakato wa kidemokrasia ulio wazi kabisa chini ya uchunguzi wa kimataifa.”
Wakati mamia ya maelfu ya watu wakiandamana Munich, Toronto, Melbourne, na Los Angeles siku ya Jumamosi kuunga mkono hatua za kimataifa dhidi ya Tehran, alisema “anajivunia wenzake, ndani na nje ya nchi, ambao wanaonyesha umoja usio na kifani na uungwaji mkono wa pande zote.”
Wakazi wa Tehran waliimba kaulimbiu dhidi ya mamlaka kutoka madirishani na paa zao siku ya Jumapili. Kituo cha televisheni cha lugha ya Kiajemi cha Iran International, kilicho nje ya nchi, pia kilirusha picha za watu wakiimba “Hii ni vita ya mwisho, Pahlavi rudi” na “Walinzi ni wafu tu,” wakirejelea jeshi la kiitikadi la Jamhuri ya Kiislamu, Walinzi wa Mapinduzi. Shirika la habari la AFP halikuweza kuthibitisha video hizo mara moja.