Ujerumani inaona juhudi za Ufaransa katika suala la ulinzi  “hazitoshi.” Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Johann Wadephul ameitaka Ufaransa “kuweka akiba,” hasa “katika nyanja ya kijamii,” ili “kuwa na uhuru unaohitajika kufikia lengo kuu la uwezo wa ulinzi wa Ulaya.” Lengo: 5% ya Pato la Taifa lililotolewa kwa usalama ifikapo mwaka 2035, hatua iliyosukumwa na Donald Trump ndani ya NATO.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Alipoulizwa kwenye kituo cha redio cha umma Deutschlandfunk kuhusu pendekezo la rais wa Ufaransa la kufadhili uwekezaji katika ulinzi au akili bandia kupitia deni la kawaida la Ulaya, Johann Wadephul, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, hakusema maneno mengi. Emmanuel Macron “anazungumza kwa usahihi wakati wote kuhusu matarajio yetu ya uhuru wa Ulaya. Mtu yeyote anayezungumzia hilo lazima atende ipasavyo katika nchi yake.” “Juhudi zilizotolewa hadi sasa katika Jamhuri ya Ufaransa hazitoshi kufikia hili,” ametangaza.

Ahadi kuhusu ulinzi wa Ulaya

Mnamo mwezi Juni 2025, nchi 32 wanachama wa ATO ziliahidi kujitolea 5% ya Pato la Taifa lao kwa ulinzi, hatua liyosukumwa na Donald Trump. Kulingana na waziri huyo kutoka kambi ya Conservative, kuna “maendeleo yanayopaswa kufanywa” miongoni mwa majirani zake, na kwa hivyo Ufaransa lazima ifanye zaidi, hata kuweka akiba, haswa katika matumizi ya kijamii, ili “kuwa na uhuru unaohitajika kufikia lengo kuu la uwezo wa ulinzi wa Ulaya.”

Johann Wadephul kisha akasema “anasubiri kwa hamu hotuba nyingine” kutoka kwa Rais Macron, mwishoni mwa mwezi Februari 2026, ambapo anatarajiwa kujadili uhuru wa Ulaya katika masuala ya ulinzi, haswa wazo la kizuizi cha nyuklia cha Ulaya mbele ya tishio la Urusi na mvutano na Marekani.

Mzozo kati ya washirika hao wawili wa Ulaya unaongezeka

Katika Mkutano wa Usalama wa Munich mwishoni mwa wiki hii, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio alikuwa wazi: ikiwa nchi za Ulaya wanataka kuwa washirika wa Marekani, lazima wafuate njia ya Trump.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *