Kikao cha 39 cha kawaida cha Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) kilichofanyika Jumapili jijini Addis Ababa kimepitisha “Azimio la Algiers” kuhusu uhalifu wa kikoloni barani Afrika, huku pia kikiidhinisha tarehe 30 Novemba kuwa Siku ya Afrika ya Mashahidi wa Bara Afrika

Kupitishwa kwa Azimio la Algiers kunakuja kama kilele cha Mkutano wa Kimataifa wa Uhalifu wa Kikoloni Barani Afrika, uliofanyika tarehe 30 Novemba na 1 Desemba 2025 mjini Algiers. Mkutano huo ulikuwa sehemu ya utekelezaji wa maamuzi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa AU kuhusu kaulimbiu ya Umoja wa Afrika ya mwaka 2025, iliyopewa jina “Haki kwa Waafrika na Watu wa Asili ya Kiafrika Kupitia Fidia na Marekebisho ya Kihistoria.”

Viongozi wa Afrika pia waliamua kuitambua tarehe 30 Novemba kama siku ya kuwakumbuka mashahidi na waathiriwa wa biashara ya utumwa wa kuvuka Atlantiki, ukoloni, na mfumo wa ubaguzi wa rangi (apartheid), wakisisitiza kuwa kumbukumbu ya pamoja ni msingi muhimu wa utambuzi wa haki, kupatikana kwa uadilifu, na kuzuia kurudia kwa uhalifu kama hiyo katika siku zijazo.

Azimio la Algiers linazitaka nchi zilizokuwa tawala za kikoloni “kubeba kikamilifu wajibu wao wa kihistoria kwa kutambua hadharani na kwa uwazi dhuluma zilizotekelezwa.” Aidha, linatoa wito wa kuanzishwa kwa Jukwaa la Haki ya Mazingira la Afrika, litakalokuwa na jukumu la kubaini maeneo yaliyoathirika, kutathmini kiwango cha uharibifu, kusaidia nchi husika, na kuandaa mapendekezo ya bara zima kuhusu urejeshaji wa mazingira na fidia.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *