TUME ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyojitokeza wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, leo Februari 17, 2026 imekutana na Rais mstaafu wa Jumuiya ya Wanasheria Tanzania (TLS), Dkt Edward Hosea.

Mkutano huo umefanyika katika Ukumbi wa Tanganyika, uliopo katika jengo la Benki Kuu ya Tanzania (BoT), ikiwa ni sehemu ya mchakato wa Tume kukusanya maoni, ushauri na taarifa kutoka kwa viongozi mbalimbali. Hoja zilizojadiliwa ni pamoja na tathmini ya athari za matukio hayo kitaifa na kimataifa pamoja na mapendekezo ya hatua za kijamii na kisheria za kuimarisha amani na mshikamano wa kitaifa.

Kadhalika Tume imekutana na  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo ambapo walijadili tathmini ya athari za matukio hayo ndani na nje ya nchi, pamoja na mapendekezo ya hatua za kijamii na kisheria za kuimarisha amani na mshikamano wa kitaifa na kimataifa. Bado Tume inaendelea kukutana na makundi tofauti, wakiwemo waathirika, ili kukusanya ushahidi kwa ajili ya kuandaa ripoti ya kina. SOMA: Tume Yakutana Mwamunyange,Waitara

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *