
Operesheni kubwa iliyofanywa mwishoni mwa wiki iliyopita na Idara ya Uhamiaji ya Zambia katika jiji la Ndola ilisababisha kukamatwa kwa zaidi ya raia 80 wa Kongo, ambao baadhi yao walifukuzwa kutoka Zambia. Kulingana na vyanzo vya ndani, watu hawa wanatuhumiwa kuishi kinyume cha sheria nchini Zambia.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Mamlaka ya Zambia inabainisha kuwa zaidi ya watu 170 wa mataifa mbalimbali wanashukiwa kuishi nchini kinyume cha sheria. Miongoni mwao ni zaidi ya Wakongo 80, wakiwemo wakimbizi.
Operesheni hiyo, iliyoendeshwa kwa ushirikiano na idara zingine za usalama za Zambia, ililenga vitongoji kadhaa huko Ndola, ikiwa ni pamoja na Hill Crest, Mitengo, Kawama, Kansenshi, na Dola Hill.
Wakimbizi kumi na watano wenye asili ya Kongo walihamishwa kwa nguvu kwenye kambi za wakimbizi za Meheba nchini Zambia.
Wakongomani kumi watu wazima na watoto 26 wasio na vibali walifukuzwa kupitia kivuko cha mpaka cha Sakania.
Wakongomani wengine, ambao waliripotiwa kusoma nchini Zambia bila vibali halali vya ukaazi, wametakiwa kuondoka nchini.
Raia watano wa Kongo bado wako kizuizini wakisubiri uchunguzi zaidi na hatua zinazowezekana za kisheria.
Idara ya Uhamiaji ya Zambia inawakumbusha wageni wote wanaoishi Zambia kwamba lazima wazingatie sheria za uhamiaji kikamilifu. Ukiukaji wowote unaweza kusababisha kukamatwa, kufukuzwa nchini, au kuhamishwa kwa lazima.