Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amesimama nchini Ethiopia siku ya Jumanne, Februari 17, ziara yake ya kwanza tangu miaka 11 ilitopita. Yeye na Waziri Mkuu Abiy Ahmed walisaini mikataba miwili mikubwa ya kiuchumi yenye lengo la kufufua ushirikiano wa kiuchumi na usalama kati ya Uturuki na Ethiopia, huku kukiwa na mvutano mkubwa kati ya Addis Ababa na Asmara.

Imechapishwa:

Dakika 3 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Kama sehemu ya ziara ambayo pia ilimpeleka Saudi Arabia na Misri, rais wa Uturuki pia alisimama nchini Ethiopia siku ya Jumanne, Februari 17, kusherehekea kumbukumbu ya miaka 100 ya kuanzishwa kwa uhusiano rasmi wa kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili.

Rais wa Uturuki alipokelewa kwa shangwe, vifijo na nderemo, katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Addis Ababa na viongozi mbalimbali vikiwemo vikosi mbalimbali vya jeshi na polisi, na gwaride la kijeshi, na alichangia chakula na viongozi wa Ethiopia katika Jumba la Kitaifa lililofanyiwa ukarabati hivi karibuni—kasri la zamani la kifalme la Haile Selassie—yote yalikuwa sehemu ya makaribisho makubwa ambayo Recep Tayyip Erdogan alipokea, njia ya kuonyesha kwa kwa Addis Ababa umuhimu wa ziara hii ya kwanza ya rais wa Uturuki tangu miaka 11 iliyopita.

Kulingana na Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed, ambaye alisifu “urafiki wa kudumu” na “ushirikiano imara” kati ya Uturuki na Ethiopia kwenye ukurasa wake ya Twitter, viongozi hao wawili walifanya majadiliano ya kina ili kufufua ushirikiano wao wa kiuchumi na usalama dhidi ya hali ya mvutano ulioongezeka kati ya Addis Ababa na Asmara, anaripoti mwandishi wetu Marlène Panara.

Viongozi wote wawili walichukua fursa hiyo kusaini mikataba miwili mikubwa ya kiuchumi, haswa katika sekta ya nishati. “Uturuki inajaribu kujiweka kama mshirika wa kimkakati wa Ethiopia, haswa katika sekta ya umeme, ambapo Ankara inaangazia ujuzi na utaalamu wake. Kwa Uturuki, fursa hiyo ni kubwa zaidi kwa sababu, sambamba, Ethiopia inataka kuendeleza sekta hii zaidi ya Bwawa Kuu la Renaissance la Ethiopia,” anaelezea Federico Donelli, profesa wa mahusiano ya kimataifa katika Chuo Kikuu cha Trieste.

Kwa karibu dola bilioni mbili na nusu zilizowekezwa nchini Ethiopia mnamo mwaka wa 2025, Uturuki pia ni mwekezaji wa pili mkubwa wa kigeni nchini humo baada ya China.

“Ni dhahiri kwamba Ethiopia inajaribu kupata silaha kutoka Uturuki”

Lakini ingawa ziara hii ya rais wa Uturuki inakuja wakati ambapo mvutano unaongezeka tena kati ya Ethiopia na Eritrea, pia inazua swali: kwa kumwalika Recep Tayyip Erdogan huko Addis Ababa, je, Abiy Ahmed hajaribu tena kuimarisha silaha zake za kijeshi kwa vifaa vya Uturuki, kama vile Ethiopia ilipopata ndege zisizo na rubani za Uturuki wakati wa vita vya Tigray mwaka wa 2021?

“Tangu vita vya Tigray, serikali ya Uturuki imekuwa ikiipa serikali ya Ethiopia wafanyakazi na vifaa vya ndege zisizo na rubani.” “Ingawa kwa sasa kuna mgogoro huko Oromia, katika eneo la Amhara, pamoja na mwingine, haujalipuka, na vikosi vya Tigray, ni wazi kwamba serikali ya Ethiopia inajaribu kupata silaha kutoka Uturuki,” alijibu Esayas Bamlack Bishaw, mtafiti huru aliyebobea katika uhusiano wa Uturuki na Ethiopia.

Kwa upande wake, rais wa Uturuki pia alizungumzia hali katika Pembe ya Afrika, akisema kwanza kwamba nchi za eneo hilo lazima zitatue matatizo yao miongoni mwao ili zisiwe “uwanja wa mataifa ya kigeni.” Kisha akachukua fursa hiyo kukosoa tena utambuzi wa Israel wa Somaliland mwezi Desemba iliyopita, akitangaza kwamba hii “haitainufaisha Somaliland wala Pembe ya Afrika”… ingawa Ethiopia inadumisha uhusiano wa karibu na eneo hili la Somalia linalotaka kujitenga.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *