
Wachimbaji 38 wa madini waliuawa wakati gesi ilipolipuka kwenye shimo katika jimbo la Plateau katikati mwa Nigeria, Wengine 27 walijeruhiwa katika mlipuko huo kwenye eneo la uchimbaji madini la Kampanin Zurak katika wilaya ya Bashar katika jimbo la Plateau.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Mlipuko huo ulitokea mapema Februari 18, na Ulitokana na uvujaji wa gesi, na monoksidi kaboni ilienea kupitia handaki za chini ya ardhi zenye hewa hafifu. Wachimbaji hao, wapatao thelathini kwa idadi na wenye umri kati ya miaka 20 na 35, walikuwa chini ya shimoni. Vifo vyao vinaaminika kusababishwa na kuvuta gesi hii yenye sumu, kulingana na ripoti ya siri iliovuja.
Sauti ya mlipuko huo ilisikika katika maeneo ya uchimbaji madini ya jirani, ambapo wachimbaji kadhaa walikimbilia eneo la tukio. Eneo hili, ndani ya Eneo la Serikali ya Mitaa ya Wase la Jimbo la Plateau katikati mwa Nigeria, ni kitovu cha kihistoria cha uzalishaji wa madini nchini.
Hata hivyo, katika miaka ya hivi karibuni, uzalishaji umepungua sana, na sasa ni migodi michache inayoendelea bila vibali iliyosalia. Kwa upande mwingine, vyombo vya habari vya ndani vinaripoti kwamba mgodi wa Kampanin Zurak unaendeshwa kisheria na kampuni ya Nigeria ya Solid Unit Nigeria Limited.
Ili kuangazia mazingira ya janga hili, Waziri wa Mazingira ameanzisha uchunguzi. Wakati huo huo, shughuli zote za uchimbaji madini zimesimamishwa katika eneo hilo.
Ajali mbaya kama hii ni za mara kwa mara nchini Nigeria. Wiki iliyopita, maporomoko ya mawe yaliwaua wachimbaji watatu katika Jimbo la Ebonyi, kusini mwa nchi.
Mnamo Septemba 2025, wachimbaji kumi na wanane walipoteza maisha yao katika Jimbo la Zamfara, kaskazini magharibi mwa Nigeria, baada ya kipindi cha mvua kubwa. Jiwe kubwa lilianguka kwenye mgodi haramu, na kuua watu 18.