Wakati wa machafuko umezuka wakati wa mkutano wa seneta wa Nairobi Edwin Sifuna na timu yake ya Linda Mwananchi huko Kakamega.

Hii ilitokea muda mfupi baada ya mtungi wa gesi ya kutoa machozi kudaiwa kutumwa na polisi wakati Sifuna alipokuwa akianza hotuba yake katika Viwanja vya Amalemba.

Sifuna aliwasihi wakazi kuwa watulivu kwani aliapa kwamba hawatalazimishwa kumaliza mkutano wao kama ilivyotokea Kitengela.

“Hatutoroki leo! Zima hiyo kitu mkutano iendelee. Hatutoroki leo. Hatutoroki leo. Zima hiyo kitu. Funika na jacket. Mkutano lazima itaendelea. Tuendelee tusiendelee. Leo hatutoroki. Zima hiyo kitu. Mrudi! Leo hakuna mkutano inaisha. Haizwezekani. Piga ingine kama uko nayo. Hakuna mtu anaharibu huu mkutano leo. Mnaniona vizuri. Mimi ndio Sifuna!” seneta huyo alisema.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *