Nchini Gambia, serikali inasema “ina wasiwasi mkubwa” kuhusu raia ambao wameenda nje ya nchi kupigana, wakikusudia “kujiandikisha katika migogoro ya silaha.”

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Maelezo haya kutoka kwa serikali ya Gambia yanakuja baada ya ufichuzi katika vyombo vya habari vya ndani kwamba hadi Wagambia 26 wameripotiwa kuuawa katika uwanja wa vita nchini Ukraine. Hata hivyo, taarifa rasmi ya serikali haitaji Urusi au Ukraine, wala majeruhi wowote wanaowezekana.

Mtetezi wa haki za binadamu Madi Jobarteh alichapisha makala ya maoni akiitaka serikali kulinda haki za raia wa Gambia walioajiriwa nchini Urusi. “Serikali haikukusudia kushughulikia suala hili. Ilijibu kwa sababu jambo hilo limewekwa hadharani,” anaeleza.

“Umaskini, ukosefu wa fursa, kukata tamaa…” 

Katika makala yake ya maoni, Madi Jobarteh anafuatilia safari ya wahamiaji hawa wasio na vibali halali wanaovuka Sahara au kujaribu njia ya Atlantiki, wakihatarisha maisha yao. “Leo, tunaona jambo baya zaidi: Wagambia wakiondoka nchini na kwenda kupigana nje ya nchi, wakifananishwa na mamluki. Chanzo cha watu kuondoka, ni umaskini, ukosefu wa fursa, kukata tamaa…” mtetezi wa haki za binadamu anasema.

“Ikiwa serikali itaedelea kukaa kimya, pia, kwa maoni yangu, ni kwa sababu inadumisha uhusiano mzuri na Urusi na inataka kuwahifadhi. Na vipi kuhusu familia katika haya yote? Wale ambao wapendwa wao wamefariki nchini Urusi? Ni msaada gani wa kisaikolojia unaopangwa? Katika taarifa yake, serikali hata haitaji familia hizi. Inatoa hisia kwamba, kwa mamlaka, jambo hilo tayari limefungwa. Inasikitisha sana,” analalama Madi Jobarteh.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *