Wakati Rais wa Marekani Donald Trump akiendelea kutishia kushambulia Iran, mamlaka ya Iran imesema kwamba itawasilisha mapendekezo mapya ya kufikia makubaliano kuhusu suala la nyuklia wakati wa duru ya tatu ya mazungumzo itakayofanyika siku ya Alhamisi, Februari 26, huko Geneva. Lakini, hwakati Israel ikizidi kuwa na wasiwasi, dalili mbalimbali zinaongeza hofu ya kuongezeka kwa mgogoro na mzozo katika eneo hilo.

Imechapishwa:

Dakika 3 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amebainisha kwamba Tehran inafanya kazi kwa bidii kwenye pendekezo jipya litakalowasilishwa siku ya Alhamisi, Februari 26, kwa Mjumbe Maalum wa Marekani, Steve Witkoff.

Wakishikilia maneno ya Marekani, ambao lazima watathmini uhalali wa mapendekezo haya, wahusika mbalimbali katika eneo hilo wanaogopa mzozo katika Mashariki ya Kati, huku Israel ikiendelea na ushawishi wake wakati duru hii ya tatu ya mazungumzo huko Geneva ikikaribia.

Kama Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghachi amesema kwamba baadhi ya vifungu vinavyohitajika na Marekani vitatimizwa, kutatua baadhi ya mambo yanayoweza kukwama itakuwa vigumu. Tehran sasa inasema iko tayari kupunguza kiwango chake cha urutubishaji wa uranium kama dhamana ya hali ya amani ya mpango wake. Mpango ambao, kwa sasa, unachukuliwa kuwa halali na mamlaka za Iran.

Hata hivyo, Steve Witkoff amesema kwamba Rais Trump anaitaka Iran iache tu mpango wake wa urutubishaji wa uranium. Akiba ya madini mazito yaliyorutubishwa, yenye jumla ya tani 10 za nyenzo ikiwemo kilo 400 iliyorutubishwa hadi 60%, ingelazimika kutumwa nje ya nchi.

Inabaki kuonekana kama, siku ya Alhamisi, Marekani na Iran watapata msingi wa pamoja… kwa gharama ya Israel ambayo inasikitika kwamba Washington haikudai dhamana kuhusu mpango wa makombora ya balistiki wa Tehran, anaripoti mwandishi wetu huko Jerusalemu, Michel Paul. Kwa kukatishwa tamaa na mkakati wa Marekani, Tel Aviv inaamini kwamba Tehran inajiimarisha, na kwamba kila siku wajumbe wake wanaposhiriki vikao huo Geneva ni siku fursa ambayo inakuwa imetolewa kwa Iran ili kuimarisha zaidi maeneo yake ya nyuklia.

Mvutano unaonekana katika miji mikuu

Zaidi ya hayo, mvutano umeongezeka katika mji mkuu wa Iran. Wairan wengi sasa wana uhakika kwamba shambulio la Marekani haliepukiki. Lakini hakuna hofu au kukimbilia madukani kununua vifaa iwapo kutatokea mgogoro, amesema mwandishi wetu huko Tehran, Siavosh Ghazi.

Kulingana na vyanzo kadhaa, Donald Trump sasa anaelekea kwenye shambulio “dogo” katika siku zijazo ili kulazimisha Tehran kusalimu amri, hata kutishia kupindua utawala ikiwa utashindwa. Chaguo linalotarajiwa na baadhi ya Wairan—baada ya mauaji ambayo nchi hiyo imeyapitia—hali ambayo inaweza kuitumbukiza nchi katika machafuko na matokeo mabaya ya kiuchumi.

Hata hivyo, mkuu wa jeshi alitangaza kwamba vikosi vya jeshi viko macho sana. Kwa upande wake, waziri wa mambo ya nje wa Iran alisema kwamba Iran itajibu shambulio lolote la kijeshi kwa kulenga kambi za Marekani pamoja na vikosi vya majini vilivyowekwa katika eneo hilo.

Hali ya tahadhari inayoshirikiwa na Lebanon, ambayo inaogopa kuingizwa katika vita vinavyowezekana vya Iran na Marekani, anaripoti mwandishi wetu huko Beirut, Paul Khalife. Naim Qassem, mkuu wa Hezbollah, mshirika wa Tehran, ameonya kwamba chama chake hakitabaki bila kuegemea upande wowote iwapo kutatokea mzozo.

Tahadhari ya Juu kwa Wamarekani waliopo nchini Lebanon

Kwa siku chache zilizopita, wanajeshi wa Marekani walioko nchini chini ya makubaliano ya ushirikiano na jeshi la Lebanon wamekuwa macho kabisa. Vyanzo vya usalama vya Lebanon vinabainisha kwamba vikosi hivi, vilivyowekwa katika kambi ya wanajeshi kilomita 50 kaskazini mwa Beirut na katika eneo kubwa la ubalozi wa Marekani kilomita 15 kutoka mji mkuu, vimeanzisha itifaki maalum ya usalama.

Hatua zilizochukuliwa na jeshi la Marekani haziendani tena na makubaliano yaliyofikiwa na mamlaka ya Lebanon. Matokeo yake, wanajeshi wa Marekani na Lebanon walipambana siku ya Jumatatu, Februari 16, nje ya kambi ya wanajeshi ya Hamat.

Kuongezeka kwa mashambulizi ya Israel pia kunaonekana kama ishara ya mzozo unaokaribia wa Iran na Marekani. Wanachama kumi na wawili wa Hezbollah, akiwemo kamanda mkuu, waliuawa wiki iliyopita katika mashambulizi ya Israel kusini na Bonde la Bekaa.

Israel inaona hii kama fursa ya kuvunja mhimili wa Iran. Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu anawaandaa mawaziri wake kwa hali yoyote inayoweza kutokea.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *