- Beatrice Wanjiru alikaribishwa kishujaa na wanakijiji na familia yake baada ya kuachiliwa kutoka gerezani, ambapo alitumikia kifungo chake kwa miaka 27
- Wanjiru alifungwa mwaka wa 1999 baada ya kupatikana na hatia ya mauaji na awali alihukumiwa kifo, lakini mahakama baadaye ilibatilisha hukumu yake
- Mwanamke huyo wa Kirinyaga alifunguka kuhusu maisha ya gerezani na kushiriki mipango yake kufuatia kuachiliwa kwake kutoka katika Gereza la Wanawake la Meru
Wakaazi wa kijiji cha Kirogo eneo la Mwea kaunti ya Kirinyaga walikusanyika kumkaribisha mmoja wao baada ya miaka mingi.

Source: Instagram
Hatimaye Beatrice Wanjiru alirejea nyumbani baada ya takriban miongo mitatu, majirani na marafiki walisherehekea kurejea kwake kwa ajabu.
Alikuwa amehukumiwa kifo mwaka wa 1999 kufuatia kesi ya mauaji iliyohusisha mtu wa karibu wa familia yake, na hivyo kumuacha akiwa hana matumaini.
Beatrice Wanjiru aliondoka lini gerezani?
Hata hivyo, hukumu yake ilipunguzwa baadaye baada ya uamuzi wa mahakama, na kumpa nafasi nyingine ya maisha.
“Nilikuwa nimehukumiwa kifo. Nilimlilia Mungu, naye akasikia kilio changu. Alinisaidia kutoka mahali hapo. Baadaye nilihukumiwa kifungo cha maisha. Niliposikia hivyo, nilipoteza matumaini. Ghafla, Mungu alinijia tena. Nilirudishwa mahakamani, na hukumu yangu ikapunguzwa,” alishiriki kwa furaha.
Wanjiru alisema ukosefu wa mashahidi waliomtetea wakati wa kesi hiyo uliathiri pakubwa hatma ya kesi yake.
Alijieleza kuwa “mgeni wa serikali” kwa miaka 27 hadi alipoachiliwa kutoka Gereza la Wanawake la Meru mnamo Ijumaa, Februari 20, kwa uhalifu anaoshikilia kuwa hakufanya.
Beatrice Wanjiru azungumza baada ya kutoka gerezani
“Nafsi yangu imejaa msamaha. Nimesamehe kila mtu, na sina kinyongo na mtu yeyote. Mungu amenifundisha mambo mengi. Nimesoma kozi kadhaa na kupata zaidi ya vyeti 30,” alisema.
Kurudi kwake hakukuwa tu na nyimbo na dansi bali pia na karamu ya kusherehekea huku wanakijiji wakishiriki furaha ya kumkaribisha nyumbani kwake.
Familia yake ilishindwa kuzuia hisia zake ilipoungana naye baada ya zaidi ya miongo miwili na nusu.
“Kama familia, tumeteseka sana, lakini kuanzia leo na kuendelea, maisha yetu yataendelea kama ya wengine ambao wamelelewa na wazazi wote wawili,” jamaa mmoja alisema.
Familia ya Beatrice Wanjiru yazungumza
Mwanafamilia mwingine alionyesha furaha yake, akibainisha kuwa hajawahi kumuona tangu azaliwe, na kufanya muungano huo kuwa wakati wa kubadilisha maisha.
“Tuliposikia kwamba anarudi nyumbani, tulifurahi sana. Tunashukuru serikali kwa kumrejesha kwetu. Walishughulikia kila kitu kwa heshima,” alisema.
Wanjiru alielezea kuachiliwa kwake kama mwanzo mpya na alisema ananuia kutumia sura hii mpya kujenga upya maisha yake na kuungana tena na watoto wake wanne, aliowaacha walipokuwa wadogo.
“Nawashukuru wote walionitembelea gerezani na hata wale ambao hawakupata nafasi hiyo. Naomba tu mahali pa kukaa kwa sababu kwa sasa sina nyumba,” alisema.
“Tuliposikia kwamba anarudi nyumbani, tulifurahi sana. Tunashukuru serikali kwa kumrejesha kwetu. Walishughulikia kila kitu kwa heshima,” alisema.
Wanjiru alielezea kuachiliwa kwake kama mwanzo mpya na alisema ananuia kutumia sura hii mpya kujenga upya maisha yake na kuungana tena na watoto wake wanne, aliowaacha walipokuwa wadogo.
“Nawashukuru wote walionitembelea gerezani na hata wale ambao hawakupata nafasi hiyo. Naomba tu mahali pa kukaa kwa sababu kwa sasa sina nyumba,” alisema.

Source: Facebook
Katika kisa kingine kutoka kaunti ya Murang’a, mwanamke mmoja alishiriki tukio la kimahaba na mumewe baada ya kuachiliwa kutoka gerezani.
Kinyua alikaa kwa miaka 18 katika Gereza la Maranjau GK kufuatia kukutwa na hatia, ambayo ilimtenga na familia yake na ulimwengu wa nje.

Pia soma
Karen Nyamu Aonekana Kukasirika baada ya Kusukumwa na Umati wa Watu kwenye Video Iliyopepea
Baada ya kumaliza kifungo chake, alipokelewa kwa furaha na mke wake na wanafamilia wengine walipokuwa wakisherehekea kurudi kwake nyumbani.
Read ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.
Chanzo: TUKO.co.ke

