• Seneta Oburu Oginga alijiunga na challenge ya ‘weka mawe’ na kuwaacha wanamtandao wamepigwa na bumbuwazi
  • Challenge hiyo ilitokana na bondia Mbavu Destroyer kabla ya pambano lake na mpinzani wake Majembe
  • Oburu aliibua challenge hiyo huku mwanadada akiwa ameshika mwamba wa zege na kuongeza neno la Gen Z ngumi ni mbwekse

Kiongozi wa chama cha ODM Oburu Oginga amewavunja mbavu wanamtandao baada ya kuchangamkia challenge ya ‘weka mawe’.

oburu
Oburu Oginga akifufua upya video ya Mbavu Destroyer. Picha: Mbavu Destroyer na Oburu Oginga.
Source: Facebook

Challenge hiyo ilivuma wiki chache zilizopita baada ya bondia Mbavu Destroyer kuitumia kumtumia vitisho mpinzani wake Majembe kabla ya mchezo wao ujao wa ndondi.

Katika video hiyo ya awali, Mbavu Destroyer alimwagiza mpinzani wake kuweka jiwe begani mwake kwa njia ya kurudia kama alivyomwambia, ‘weka mawe’.

Oburu amekuwa akisambazwa sana na hotuba zake za kisiasa tangu alipopandishwa cheo na kuwa kinara wa ODM.

Oburu awasha mtandao na challenge ya ‘weka mawe’

Katika toleo la hivi punde zaidi, ametamba na challenge ya ‘weka mawe’. Kama inavyoonekana kwenye klipu hiyo, Oburu, aliyepewa jina la utani Kiongozi wa Vijana, aliruka juu ya mtindo huo na mwanadada aliyebeba kipande cha block na kumfanya seneta wa Siaya kusema ‘weka mawe.’

Pia soma

Magazetini: Mipasuko Upinzani huku Matiang’i Akituhumiwa Kuwa Mradi wa Ruto

Oburu aliongeza ishara nyingine ya Gen Z ya ngumi ni mbwekse.

Video hiyo ilisambaa kama moto na kuvutia maoni ya wanamtandao.

Francis Mwgela: “Anahitaji pawa, anataka mbavu.”

Lenna Nkatha Muriuki: “Mnasumbua Gen Z wetu.”

Marcelo Salah: “Mnasumbua youth leader.”

Calvin Josh: “Weka mawe kabisaaa bila break. Tafuta mawe kubwaa sana uwekelee bila kutoa.”

Eugine Muyale: “Weeee pole pole… Bado tunahitaji youth leader ako na paaaawaaa.”

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *