
Ingawa ripoti ya hivi karibuni kutoka kwa idara ya ujasusi ya Kenya inaonyesha kwamba zaidi ya Wakenya 1,000 waliajiriwa na jeshi la Urusi, mara nyingi kwa njia ya udanganyifu, nchini Afrika Kusini, ofisi ya rais imetangaza siku ya Jumanne, Februari 24, kurejeshwa nyumbani kwa Waafrika Kusini 17 ambao pia walikuwa wameajiriwa kinyume matakwa yao kupigana vitani nchini Ukraine.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Na mwandishi wetu huko Johannesburg, Josephine Kloeckner
Kwa miezi kadhaa, walikuwa wakiomba msaada kutoka nchi yao, wakidai kwamba wako mstari wa mbele nchini Ukraine baada ya kutapeliwa. Katikati ya shutuma zao: binti wa rais wa zamani Jacob Zuma anayooshewa kidole.
Nchini Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa amemshukuru Vladimir Putin katika taarifa kwa kuruhusu kurejea nyumbani kwa Waafrika Kusini 17 kutoka mstari wa mbele nchini Ukraine. “Rais Ramaphosa alitoa shukrani zake za dhati kwa Rais wa Urusi Vladimir Putin, ambaye aliitikia vyema ombi lake la kurejeshwa kwa watu hawa nchini mwao,” ofisi ya rais imesema katika taarifa. Wanne kati yao walirejeshwa nyumbani wiki iliyopita, na wengine 11 wanakaribia kurejeshwa.
Watu hawa, wenye umri wa kati ya miaka 20 na 39, walitumia miezi saba katika eneo la Ukraine. Kulingana na ushuhuda wao, walitumwa Urusi mnamo mwezi Julai 2025 kwa kile walichoamini kingekuwa mafunzo ya walinzi. Lakini walipofika, walijikuta wameajiriwa jeshini na kutumwa vitani.
Chama cha rais wa zamani Zuma cha MK katika migogoro ya familia
Mnamo mwezi Novemba, maombi yao ya msaada yalifikia vyombo vya habari vya Afrika Kusini, na kisha serikali. Wanaume hao na familia zao wanalaani kuhusika kwa Mkhonto we Sizwe, MK iliyofupishwa, chama cha rais wa zamani Jacob Zuma, ambaye aling’olewa madarakani kutokana na ufisadi mnamo mwaka 2018, na haswa binti yake, Duduzile Zuma, ambaye inadaiwa aliwahimiza kushiriki katika kile alichokiita mafunzo ya walinzi.
Kutokana na utata huo, alijiuzulu mara moja kutoka nafasi yake kama mbunge. Chama kinakana kuhusika mada hayo.
Kufanya kazi kama mamluki au kupigania serikali nyingine ni kinyume cha sheria nchini Afrika Kusini, isipokuwa kwa idhini ya serikali. Uchunguzi kuhusu mazingira ya kuajiriwa huko kinyume cha sheria unaendelea, kulingana na ofisi ya rais wa Afrika Kusini.