Baada ya miezi kadhaa ya uchunguzi, wabunge wa Marekani wamewasilisha ripoti kuhusu madai ya mateso ya Wakristo nchini Nigeria katika Ikulu ya White House siku ya Jumatatu, Februari 24. Waraka huo uliowasilishwa na wanachama wa mrengo wa kulia wa Kikristo, unarudia madai yanayoonekana kuwa “hayana msingi” na waangalizi kadhaa na kutoa wito wa vikwazo vinavyolenga watu binafsi na makundi fulani yanayoshutumiwa kuzuia uhuru wa kidini nchini humo.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Mapendekezo haya yanafuatia uchunguzi na mfululizo wa mashauriano yaliyofanywa mwishoni mwa mwaka 2025, nchini Nigeria na Washington, na wanachama wa Bunge la Marekani.

Katika hitimisho lao, wabunge wa Marekani wanarudia kwamba Wakristo ndio waathiriwa wakuu wa vurugu nchini Nigeria, hali wanayoielezea kama “mateso.” Hati hii inaelezea “vitendo halisi” vingezingatiwa ili “kukomesha hali hii,” anaelezea Mbunge Riley Moore kwenye ukurasa wake mtandao wa kijamii wa X (zamani Twitter).

Ripoti hiyo inawahusisha haswa “wanamgambo wa Fulani,” ikiwashutumu kuhusika katika vurugu hizo. Wabunge wa Marekani wanapendekeza kupokonywa silaha na kurejeshwa katika maisha ya kiraia.

Waandishi wa ripoti hiyo pia wanawashutumu badhi ya wafanyabiashara kutoka China kwa kufadhili baadhi ya makundi yenye silaha ili kuwezesha uchimbaji haramu wa amana za madini kaskazini magharibi mwa Nigeria.

Katika muktadha huu, mwakilishi kutoka Wizara ya Fedha ya Marekani kwa sasa yuko nchini Nigeria kujadili kupambana na ufadhili wa ugaidi.

“Kuwanyamazisha Wakristo wachache”

Wabunge wa Marekani pia wanatoa wito wa kufutwa kwa sheria ya Kiislamu, ambayo inatumika katika majimbo kadhaa yenye Waislamu wengi kaskazini mwa Nigeria, ambapo inaendana na sheria ya kawaida. Wanabaini, haswa, kwamba sheria za kufuru zinatumika “kuwanyamazisha na kuwalenga Wakristo wachache” katika maeneo haya.

Hatimaye, wabunge wa Marekani wanatetea kuimarisha ushirikiano wa Nigeria na washirika wake wa kimataifa, haswa katika mapambano dhidi ya ugaidi.

Tangu mwezi Oktoba 2025, Washington imeiweka Abuja tena kwenye orodha yake ya nchi “zinazotia wasiwasi sana” kuhusu uhuru wa kidini. Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa anasema kwamba 80% ya vurugu dhidi ya Wakristo duniani kote zimejikita nchini Nigeria.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *