WAZIRI wa Fedha Balozi Khamis Mussa Omar amewaagiza  viongozi wa Mamlaka ya Mapato  Tanzania (TRA) kuendelea kuwa wabuni katika ukusanyaji wa mapato nchini. Akishiriki hafla ya futari iliyoandaliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) jijini Dar-es-salaam , Balozi  Omar  amesema serikali inampango wa kuendelea kuhamasisha makusanyo ya mapato katika maeneo mengine mikoani.

“ Hapa Dar-es-salaam  inabidi kwa sasa tuache kidogo tumefanya sana hapa na sasa ni kwenda maeneo mengine Tanzania ili lengo la serikali liweze kutimia la ukusanyaji wa mapato kwa nchi nzima”, alisema Balozi Omar. SOMA: Naibu Waziri Fedha azindua boti ya TRA

Balozi Omar alikua na ziara ya kikazi ya siku mbili katika Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), jijini Dar es Salaam, ambapo alikagua na kujionea utekelezaji wa shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na mamlaka hiyo hususan katika kukuza mapato ya Serikali kwa njia ya ukusanyaji wa kodi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *