• Samson Mutua ndiye Mkenya wa kwanza kupokea sindano ya chanjo ya kuzuia maambikizi ya VVU ya Lenacapavir ambayo itawazuia watu walio katika hatari ya kupata ugonjwa huo kwa miezi sita
  • Waziri wa Afya Aden Duale alizindua uzinduzi wa kitaifa wa PrEP ya sindano ya muda mrefu ya kuzuia maambukizi ya VVU, na wote walishuhudia Mutua akipokea chanjo hiyo
  • Wakenya walielezea hisia tofauti kuhusu kuanzishwa kwa Lenacapavir katika juhudi za kuzuia maambukizi ya VVU, huku wengine wakitamani kuipata huku wengine wakiogopa kuwa ‘panya wa maabara’

Nairobi, Kenya: Mchukuzi wa kutumia bodaboda mwenye umri wa miaka 27 mtaani Kawangware, kwa jina Samson Mutua ndiye Mkenya wa kwanza kupokea chanjo ya muda mrefu ya kuzuia maambukizi ya VVU, Lenacapavir.

Samson Mutua taking the pills.
Samsom Mutua akimeza vidonge. Ni Mkenya wa kwanza kuvipokea. Picha: MoH.
Source: Facebook

Yanayoendelea Sasa: ​​Waziri wa Afya Mhe. Aden Duale alizindua dawa ya kuzuia maambukizi ya VVU kwa sindano (PrEP), Lenacapavir, inayotumika kwa muda mrefu, ikiwa ni awamu ya kwanza ya uzinduzi wa kitaifa na kuimarisha dhamira ya Kenya ya kukomesha janga la VVU kupitia suluhisho bunifu za kinga zinazolenga watu.

Pia soma

Edwin Sifuna aongezwa muda kuendelea kuwa Katibu Mkuu wa ODM, hatua ya kumng’atua yazuiwa

Mutua alidungwa sindano mbili za Lenacapavir kwenye tumbo lake la chini katika Kituo cha Afya cha Riruta saa 8 asubuhi, na Waziri wa Afya Aden Duale alikuwepo kushuhudia.

Baada ya sindano hiyo, Mutua alilazimika kumeza vidonge viwili vya Prep mara moja ili kuhakikisha kwamba alikuwa amekingwa kwa siku ya kwanza. Atachukua vidonge viwili zaidi leo, Ijumaa, Februari 27. Hiyo ina maana kwamba amelindwa dhidi ya VVU kwa miezi sita ijayo, baada ya hapo atarudi kwa sindano nyingine.

Mutua hatatumia vidonge vingine vya Prep ndani ya miezi hiyo sita.

The tablets to prevent HIV.
Chanjo ambayo inazuia kwa muda mrefu maaambukizi ya VVU. Picha: MoH.
Source: Facebook

Unahitaji kujua nini kuhusu Lenacapavir?

Lenacapavir inasifiwa kama sindano ya muda mrefu inayofanya kazi kwa ajili ya kuzuia VVU, katika hatua kubwa ya kupunguza maambukizi mapya na kuimarisha mwitikio wa kitaifa wa VVU.

Akizungumza katika Kituo cha Afya cha Riruta jijini Nairobi, Waziri huyo alielezea kuanzishwa kwa Lenacapavir kama hatua muhimu katika juhudi za kuzuia, akibainisha kuwa Wakenya milioni 1.4 wanaishi na VVU, huku maelfu ya maambukizi mapya yakirekodiwa kila mwaka.

Alisisitiza kwamba kupanua chaguzi bunifu za kinga ni muhimu katika kupunguza mwenendo wa maambukizi na kulinda idadi ya watu walio katika mazingira magumu.

Pia soma

Edwin Sifuna ni kama mafuriko yasiyoweza kuzuilika kwa mikono, wakili amwambia Ruto kuhusu 2027

Kulingana na Duale, dawa hiyo ni salama kwa matumizi, kwani imekidhi mahitaji yote ya kisheria na ununuzi chini ya sheria za kitaifa na miongozo ya afya.

Usalama, ubora, na ufanisi wa dawa hizo pia zilitathminiwa kwa kina kupitia mapitio ya kisayansi ya kimataifa na tathmini ya ndani na Bodi ya Dawa na Sumu, kwa usaidizi kutoka kwa Mfuko wa Kimataifa.

Sindano hiyo itatolewa mara mbili kwa mwaka na kutolewa bure kwa watu wanaostahiki katika vituo vya afya vya umma vilivyochaguliwa katika kaunti za kipaumbele.

Sindano hiyo itatolewa mara mbili kwa mwaka na kutolewa bure kwa watu wanaostahiki katika vituo vya afya vya umma vilivyochaguliwa katika kaunti za kipaumbele.

“Uzinduzi wake utafuata mbinu iliyopangwa kwa awamu na inayoongozwa na wataalamu wa afya waliofunzwa ili kuhakikisha upatikanaji salama na usawa,” ilisema Wizara ya Afya kwenye ukurasa wake wa Facebook.

Wakenya walisema nini kluhusu maendeleo hayo mapya?

Chemutai Kipkorir:

“Chanjo ni salama mradi tu watu wapate elimu mapema. Natumai si lazima pia kwa sababu watu wana haki ya kukataa na kuchagua. Ninavutiwa tu kwa sababu dawa hiyo hiyo haitumiki katika nchi zinazoitengeneza.”

Pia soma

Magazeti ya Kenya: NIS yamhusisha mwanachama wa UDA na sakata ya Wakenya kuingia jeshi la Urusi

Absolom Kiarie:

“Nyaboke Ndege keep serving wananchi. Good job.”

Copen Wa Njoroge

“Are those watching already vaccinated.”

Wakang’ethe Mûnjirû:

“Is it in just Kenya and mostly Africans? Ama there’s cure for AIDS already? Anyway watu wadungwe na wakunywe dawa sijaongea mimi.”

Nduku Wa Lamu:

“Huko imetoka wamedungwa? Ama testing goes with us… siwezi.”

RickyJohn Efekt Nganga:

“Walitumia criteria gani? Alisema nini ama ako na partner HIV positive? I’m just overthinking don’t slap me.”

Ukweli wa Serikali kwa Vijana Wanaoishi na VVU

Katika hadithi iliyopita, serikali ya Kenya ilishiriki mpango thabiti wa kukomesha VVU na UKIMWI kama tishio la umma ifikapo 2030, lakini changamoto nyingi zinazoendelea zinatishia kufikiwa kwa lengo hili.

Siku ya UKIMWI Duniani huadhimishwa Desemba 1, kote ulimwenguni, na ni hasa kuadhimisha maisha yaliyopotea, kusherehekea maendeleo katika mikakati ya kukabiliana na janga na kuwasaidia waathiriwa.

Wizara ya Afya iliandaa Nusu Marathon ya Kitaifa na Tukio la Kuadhimisha Siku ya Jumapili, Novemba 30, 2025.

Pia soma

Video: Edwin Sifuna afichua kwamba mama kanisa alimpigia, akamkemea kwa kutumia lugha chafu Kakamega

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *