- Mbunge wa Emurua Dikirr Johana Ng’eno alifariki katika ajali ya helikopta ambayo pia iligharimu maisha ya watu wengine watano katika kaunti ya Nandi
- Video za kuhuzunisha za zimeibuka zikimuonyesha Ng’eno akitoa hotuba yake ya mwisho kabla ya kuabiri ndege iliyoharibika
- Katika video hiyo, mbunge huyo alizungumza kuhusu Uchaguzi Mkuu wa 2027, akiwataka wapiga kura kuzingatia utendakazi wa maendeleo wanapochagua viongozi
Mbunge wa Emurua Dikirr Johana Ng’eno alifariki Jumamosi, Februari 28, baada ya ajali ya helikopta katika kaunti ya Nandi.

Source: Facebook
Mbunge huyo alikuwa miongoni mwa watu sita waliopoteza maisha wakati helikopta ya Airbus H125, yenye nambari ya usajili 5Y-DSB ilipoanguka na kuwaka moto katika eneo la Chepkiep huko Mosop. Vikosi vya uokoaji vilithibitisha baadaye kwamba hakukuwa na manusura wa tukio hilo.
Kufuatia mkasa huo, video ya kuhuzunisha imeibuka ikimuonyesha mbunge huyo akitoa hotuba yake ya mwisho kwa umma.
Maelezo ya hotuba ya mwisho ya Johana Ng’eno kabla ya kifo

Pia soma
Johana Ng’eno: Mandhari ya Jumba la Kifahari la Marehemu Mbunge Aliyeangamizwa na Helikopta
Video hiyo ilirekodiwa wakati wa mkutano wa kisiasa huko Endebess, ambapo Ng’eno alizungumza kuhusu uongozi, uchaguzi, na ushindani wa kisiasa wa amani kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2027.
Wakati wa hotuba hiyo, Ng’eno alisisitiza kuwa uchaguzi wa 2027 huenda ukaamuliwa na utendakazi wa maendeleo badala ya siasa za utu.
Aliwahimiza viongozi kujikita katika kufikisha huduma kwa wananchi badala ya kutegemea umaarufu au ujuzi wa kuzungumza hadharani.
“Hakuna mtu ambaye atachaguliwa tena kulingana na sura yake, au kama anajua kuzungumza sana. Utapewa kura tu kulingana na kazi uliyofanya,” alisema.
Ng’eno pia alizungumza kuhusu kudumisha amani wakati wa kampeni za uchaguzi na kuwataka wafuasi wa kisiasa kuepuka machafuko.
Alichosema Ng’eno kuhusu Ruto katika hotuba ya mwisho
Alikumbusha mkutano huo kwamba nchi ilikuwa imesalia takriban miezi 16 kabla ya uchaguzi mkuu ujao na kutoa wito wa ushindani wa kisiasa wa amani.
Ng’eno pia alizungumza kuhusu Rais William Ruto, akisema kuwa kwa sababu ya rekodi yake ya maendeleo, kuna uwezekano mkubwa akapata muhula wa pili afisini.
“Tumesalia na takriban miezi 16 kabla ya uchaguzi ujao. Nataka tupige kura kwa amani, bila machafuko. Tunataka mchakato wa amani. Na tunajua, kutokana na kazi nzuri ambayo rais amefanya, tutampa muhula wa pili,” alisema huku umati ukipiga makofi na kushangilia.

Pia soma
Johanna Ngeno: Jumbe Zaidi Zavuja za WhatsApp Kuonyesha Ndoto Kubwa ya Mpiga Picha wa Marehemu
Mbunge huyo pia alizungumzia ushindani wa kisiasa nchini, akisema hana tatizo na wanasiasa kusafiri kote nchini Kenya kufanya kampeni za kutafuta kura.
Alimtaja aliyekuwa naibu wa rais Rigathi Gachagua kuwa mfano wa viongozi waliokuwa wakifanya kampeni katika maeneo tofauti.
“Sisi hatuna tatizo na mtu, wanaozunguka sasa hivi kama naibu rais wa zamani au waziri wa mambo ya ndani waende watembee, hakuna shida, wengine walikabidhiwa majukumu makubwa watuonyeshe wamefanya nini, siku ya uchaguzi tutampima kila mtu kulingana na kazi yake,” alisema.
Muda mfupi baada ya hotuba hiyo, helikopta ambayo baadaye ingeanguka ilionekana ikielea juu ya mkusanyiko, ikijiandaa kuondoka.
Ng’eno alikiri kwa ufupi kwamba ndege hiyo ilikuwa imeanza kusonga, lakini alichagua kumaliza matamshi yake kabla ya kuondoka. Pia alitoa mchango wa KSh 300,000 kwa hafla hiyo kabla ya kuhitimisha hotuba yake.
Read ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.
Chanzo: TUKO.co.ke